Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi, kamishna msaidizi Mtatiro Kitinkwi, amethibisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo imehusisha gari dogo la mkurungenzi wa kilwa na gari ya aina ya probox iliyobeba abiria ambapo watu wanne wamefariki dunia wakiwamo wanawake wawili, mwanaume mmoja na mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu. Chanzo cha ajali hiyo bado hakijathibitishwa.
" Ni kweli kwamba watu wanne wamefariki wakiwamo mama wawili watu wazima , mwanaume mmoja mtu mzima na mtoto mmoja wenye umri wa mwaka mmoja na nusu " amesema kamanda Kitinkwi.
0 Comments