Ticker

10/recent/ticker-posts

Washindi wa uchaguzi kwenye kura za maoni za Ubunge wa CHADEMA waliopita kwenye majimbo yao

Washindi wa uchaguzi kwenye kura za maoni za Ubunge wa CHADEMA waliopita kwenye majimbo yao ni  kama ifuatavyo:

1.Mshindi Jimbo la Kawe ni Halima Mdee mwenye kura 63  (71.5%).

2.  Tarime Mjini mshindi ni Esther Matiko mwenye kura 80 (97. 6%) 

3. Tarime Vijijini mshindi ni John Heche ambaye amepata kura 268 (99.2%) .

-Heche alikuwa Mgombea pekee na alihitaji tu kura za Ndio au Hapana, kwenye kura zilizopigwa, kura za Ndio ni 268 (99.2%),zilizoharibika ni 2 (0.74%) hakuna kura ya Hapana

4. Mshindi Jimbo la Bunda Mjini ni Ester Bulaya mwenye kura 126 

5. Jimbo la Iramba mshindi ni Jesca Kishoa mwenye kura 134 (98%) .

- Jesca alikuwa Mgombea pekee na alihitaji tu kura za Ndio au Hapana, kwenye kura 136 zilizopigwa, kura za Ndio ni 134 (98%), zilizoharibika ni 2 na hakuna kura ya Hapana.

6. Jimbo la Isimani mshindi ni Patrick Ole Sosopi mwenye kura 115 (82.6%).

7.Mshindi jimbo la Mbeya Mjini ni Joseph Mbilinyi (Sugu) mwenye kura 294

- Sugu alikuwa ni Mgombea pekee na alihitaji tu kura za Ndio au Hapana ambapo amepata Ndio 294 na Hapana 5.