Ticker

10/recent/ticker-posts

WANAFUNZI 6 KATORO WAVUNJA REKODI KWA UFAULU LICHA YA KUFANYA MTIHANI MAHABUSU.

Na Abdullatif Yunus wa Michuzi TV

Matokeo ya Kidato cha Nne 2019 yaliyotangazwa mnamo tarehe 09, Januari 2019, na Baraza la Mitihani Tanzania, yameendelea kusisimu wadau mbalimbali wa Elimu kufuatia baadhi ya Wahitimu kuonesha maajabu katika ufaulu wao.

Miongoni mwa maajabu na rekodi iliyojitokeza katika matokeo hayo, ni pamoja na waliokuwa Wanafunzi sita wa Shule ya Seminari ya Katoro iliyopo Mkoani Kagera, kufaulu kwa alama nzuri sana katika matokeo ya Mtihani huo wa kuhitimu kidato cha nne mwaka jana.

Hali hiyo imeonekana kuwashangaza walio wengi kwani si jambo rahisi sana Kwa hofu ya mtihani inavyokuwa, lakini watuhumiwa hawa wameweza kufanya vizuri baada ya kuomba nafasi hiyo Kwa mamlaka zinazohusika na kesi yao, mpaka sasa upepelezi wa kesi yao haujakamilika licha ya kuonekana wazi dalili za uonevu kulingana na mlolongo wa kesi yao ulivyo.

Wanafunzi hao ambao mpaka sasa wapo mahabusu Kwa kushikiliwa Kwa Tuhuma za kifo cha Mwanafunzi mwenzao kilichotokea miezi kadhaa iliyopita, wametambulika Kwa majina yao na ufaulu katika mabano kuwa ni Sharifu Amri (Division II.19), Fahad Abdul-Azizi (Division II.21), Hussein Mussa (Division II.21), Sharifu Uledi (Division II.21), Abdallah Ntarambe (Division III.23), na Usama Ramadhani (Division III.25).


 Pichani ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Katoro Sheikh Faharuddin Mustapha akitoa Maelezo mafupi juu ya Watuhumia 6 waliofanya vizuri katika matokeo yao, wakati wa Mahafali ya kuhitimu kidato cha Nne 2019.
 Pichani Mkuu wa Shule Katoro Islamic Seminary Sheikh Fakharuddin Mustapha akifafanua jambo, kuhusu watuhumiwa 6, wakati alipokuwa akizungumza na Michuzi Blog Ofisini kwake.
 Pichani ni sehemu ya wahitimu kidato cha Nne Katoro Islamic Seminary 2019, wakionekana katika nyuso za huzuni Mara baada ya kisomo maalum cha Dua ya kuwaombea wenzao watuhumiwa 6, wakati wa mahafali yaliyofanyika shuleni Katoro.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2t7rRab
via

Post a Comment

0 Comments