Ticker

10/recent/ticker-posts

UTALII WAANZA KUPAA JUMUIYA YA MBARANG'ANDU, NAMTUMBO.


Na Yeremias Ngerangera 
Utalii na uwindaji  wa kitalii katika jumuiyya  ya Mbarang’andu umeanza  kupaa baada ya musimu wa uwindaji  wa kitalii kuanza  julai mosi mwaka jana 2019  katika jumuiya hiyo.
Afisa wanyamapori  wa Halmashauri  ya wilaya  Namtumbo Ernest Nombo katika taarifa yake  alisema utalii wa uwindaji na utalii wa kuona  umeongezeka  katika musimu wa  julai hadi desemba  2019 ikilinganishwa na misimu miwili ya nyuma.
Bwana  Nombo alidai kuongezeka  kwa utalii katika jumuiya hiyo kumetokana  na uhifadhi wa wanyama  kukiendana na ongezeko la wanyama  wanaovutia  watalii kwenda  kuwaona na kuomba kibali cha kuwinda.
Aidha bwana Nombo amesema katika musimu wa Julai mpaka desemba 2019 jumuiya ya Hifadhi wanyamapori  kwa jamii (WMA) ya mbarang”andu inastahili kupata gawio la fedha  kutoka  TAWA kiasi  cha dola za marekani 53,817.5 na Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo kupata gawio kiasi cha dola za marekani 8,807.5.
Ofisa Ardhi  na maliasili wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo bwana Saimon Sambalu katika taarifa hiyo alidai kanuni za jumuiya za uhifadhi wanyamapori (WMAs) za mwaka 2018 kifungu cha 72(1) na (2) (b)  vinaeleza kuwa asilimia 50 ya mapato ya mwaka yatokanayo na uwindaji wa kitalii kwenye  WMA lazima yapelekwe katika vijiji vinavyounda  jumuiya husika .
Bwana Sambalu katika tarifa hiyo alisema asilimia 50 ya dola za kimarekani  53,817.5 ni sawa  na dola za kimarekani 26,908.75 ambapo kijiji cha kitanda ,Nambecha,Likuyuseka ,Songambele,Mchomoro ,Kilimasera  na Mtelamwahi vitapata kiasi cha dola za marekani 3,844.10 kila kijiji.
Halmashauri  ya wilaya ya Namtumbo ina jumla ya jumuiya  ya Hifadhi  za wanyamapori za jamii(WMAs)tatu  ikiwemo ya Kisungule,Kimbanda  pamoja na Mbarang”andu ambayo inaonekana kuwa  na idadi kubwa ya utalii katika msimu wa julai mpaka desema 2019.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/38cJd47
via

Post a Comment

0 Comments