Ticker

10/recent/ticker-posts

RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA NYUMBA ZA KWAHANI JIJINI ZANZIBAR

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mji Mpya wa Kwahani Jijini Zanzibar, (kulia kwa Rais) Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Mhe. Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa na (kushoto kwa Rais) Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar.Ndg.Khamis Mussa, ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar.Mhe.Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa, akitowa maelezo ya Ujenzi wa Mji Mpya wa Kwahani Jijini Zanzibar, wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la ujenzi huo unaofanyika katika eneo la kwahani
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mshauri Elekezi wa Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Mji Mpya Kwahani Jijini Zanzibar,kutoka Kampuni ya Arqes Africa Ltd .Rose Nestory  na (kulia kwa Rais) Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar.Mhe.Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa, ikiwa ni shamrashamra za sherehe za Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein, akitembelea Ujenzhi wa Nyumba mpya za Mji wa Kwahani Wilaya ya Magharibi Unguja ikiwa ni shamrashamra za Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Mradi huo Kwahani Jijini Zanzibar.

BAADHI ya Wageni waalikwa na Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar, wakifuatilia hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za Mji Mpya wa Kwahani Jijini Zanzibar, ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
BAADHI ya Viongozi wa Idara za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa nyumba za mji mpya wa kwahani jijini Zanzibar, ikiwa ni shamrashamra za Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar
BAADHI ya Masheha wa Shehia za Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wakifuatilia hafla ya uwekaji wa jiwe la nsingi la ujenzi wa nyumba za mji mpya wa kwahani Jijini Zanzibar, ikiwa ni shamrashamra za kusherehekea Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
KATIBU Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar.Ndg. Khamis Mussa akitowa maelezo ya Kitaalam ya Ujenzi wa Nyumba za Mji Mpya wa Kwahani Jijini Zanzibar, wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi huo, ikiwa ni shamrashamra za Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
WAZIRI wa Fedha na Mipango Zanzibar Mhe.Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa akizungumza wakati wa uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za Mji Mpya wa Kwahani Jijini Zanzibar.ikiwa ni shamrashamra za Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
BAADHI ya Wananchi wa Kwahani wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia (hayupo pichani) wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wac nyumba za mji mpya wa kwahani jijini Zanzibar, ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akihutubia wakati wa hafla ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mradi wa Nyumba za Mji Mpya wa Kwahani Jijini Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika eneo hilo la ujenzi kwahani ikiwa ni shamrashamra za Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Wananchi wa Kwahani, baada ya kumalizika kwa hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Mradi wa Nyumba za Mji Mpya  Kwahani Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)   
……………….
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein amesema kabla ya Mapinduzi ya 1964, Wazalendo wa Zanzibar walibaguliwa kwa makaazi kutokana na uwezo duni walionao.
Dk. Shein amesema hayo katika hafla ya uwekaji wa Jiwe la msingi la ujenzi wa Mji mpya wa Zanzibar eneo la Kwahani, ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Alisema wengi wa wananchi ikiwemo wafanyakazi waliishi katika maeneo ya ng’ambo kwenye makazi ya nyumba duni, huku wale wenye uwezo wakiishi katika maeneo ya mji Mkongwe na maeneo mengine ya kati ya mji.
Alisema katika uchaguzi wa mwisho wa mwaka 1963, Chama cha ASP kupitia Ilani yake ya uchaguzi kilitowa ahadi ya kuwapatia makazi bora wananchi wote, hatua iliyofuatiwa na ujenzi wa nyumba za Kikwajuni (nyumba za miguu) mara baada ya Mapinduzi kupitia msaada wa Serikali ya Watu wa Ujerumani.
Alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi chini ya Uongozi wa Marehemu  Abeid Aman Karume, iliendeleza dhamira ya kujenga nyumba bora za kisasa hatua kwa hatua,  kwa kujenga nyumba katika eneo la Kilimani na hatimae Michenzani. 
Aidha, alisema Mapinduzi ya 1964 yameondowa tofauti ya makazi iliyokuwepo kati ya mji mkongwe na ng’ambo, ambapo hivi sasa mji wote unaonekana kuwa mmoja.
Alisema Serikali ina mipango madhubuti ya kuendeleza ujenzi wa nyumba za aina hiyo katika maeneo mbali mbali ya mji ili kuunganisha mazingira yafanane na majengo ya Michenzani.
Alisema ujenzi huo utaunganisha majengo ya Michenzani Maul, eneo la packing pamoja na nyumba za Michenzani, hivyo kuleta mandhani nzuri ya mji wa Zanzibar.
Aliwahakikishia wananchi walioondoshwa kupisha ujenzi katika eneo hilo kuwa mara baada ya ujenzi kukamilika watarudi eneo hilo na kuendelea kuwa wananchi wa Kwahani.
Alisema dhamira ya Serikali ni kuijenga Kwahani mpya ili wananchi waweze kuishi katika makazi bora zaidi na kujiletea maendeleo.
Aidha, alisema mara baada ya Mapinduzi ya 1964, kuna nyumba kadhaa zilitaifishwa na kuwa mali ya Serikali,  na kubainisha kuwa Serikali kupitia uratibu wa shirika la nyumba inazifahamu nyumba zote hizo, hivyo akawataka watu kuondokana na ghilba ya kuhodhi nyumba hizo. 
Alisema ujenzi huo pamoja na mambo kadhaa ya maendeleo yanayoendelea kufanyika hapa nchini ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa  CCM ya mwaka 2015-2020.
Akigusia suala la malipo ya fidia kwa ajili ya shughuli za maendeleo, ikiwemo maeneo ya ujenzi, Dk. Shein alisisitiza kwa kusema kuwa ardhi na mali ya Serikali, hivyo akabainisha umakini wa Serikali katika kuhakikisha wananchi wote wenye haki ya kulipwa fidia wanalipwa  kutokana na mali zao na sio umiliki wa ardhi.
“Serikali inatowa haki ya kutumia ardhi lakini sio yako, ikitaka ina haki ya kumpa mtu mwengine………..”, alisema.

Nae, Waziri wa Fedha na Mipango Balozi Mohamed Ramia  alisema uendelezaji wa makazi bora kwa wananchi wa Zanzibar, ulitokana na ahadi iliyotolewa katika  Ilani ya ASP ya mwaka 1963 ya kuhakikisha wananchi wote wanaishi katika makazi bora.
Alisema hatua ya serikali ya awamu ya saba iliyo chini ya uongozi wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein ya kujenga nyumba hizo ni utekelezaji wa  mipango iliyoanzishwa na viongozi waliotangulia, akitoa mfano wa ujenzi wa nyumba za maendeleo katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba.
Alisema ujenzi wa mji mpya wa Zanzibar eneo la Kwahani  unaashiria dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kujenga miji ya kisasa katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba.
Aidha, alisema Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 inafikia kikomo mwaka huu, akabainisha matumaini yake ya kuwepo maendeeo endelevu katika miaka ijayo kwa kuzingatia urithi wa CCM kutoka vyama vya ASP na TANU.
Balozi Ramia aliushukuru Uongozi wa Shehiya ya Kwahani, CCM Mkoa Mjini Magharibi pamoja na Kamati ya Fedha ya Baraza la Wawakilishi kwa kufanya juhudi kubwa kuwahamasiha wananchi wa eneo hilo kukubali wazo la Serikali  la kuanzisha ujenzi huo.
Mapema, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Khamis Mussa, alisema ujenzi wa mji mpya wa Zanzibar eneo la Kwahani unatekelezwa kupitia Kampuni ya Estim Construction Ltd kwa gharama ya shilingi Bilioni 19.6, ambapo awamu ya kwanza ya ujenzi huo ulioanza Oktoba 2, 2019 unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 31, 2020. 
Alisema ujenzi huo utakaohusisha‘Blocks’ tatu utakuwa na  nyumba 70 za kuishi na maeneo 56 ya biashara, wakati ambapo Blocks mbili zinazofanana kila moja itakuwa na majengo mawili pacha yenye nyumba 14 kila moja pamoja na maeneo ya biashara na kufanya jumla ya nyumba 28 za kuishi .
Alisema ‘Block’ la tatu  litakuwa na jengo moja lenye nyumba 14, ambapo kila nyumba itakuwa na vyumba vitatu vya kuishi, jiko, choo, stoo pamoja na ukumbi.
Aidha, alisema kila jengo litakuwa la ghorofa sita, sambamba na mji huo kuwa na barabara za ndani, matangi mawili ya maji pamoja na huduma za umeme.
Mussa alisema  kuwa mradi huo umezingatia utekelezaji wa Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini MKUZA 111 pamoja na Ilani ya CCM ya 2015-2020. 
Alisema kufuatia ujenzi huo nyumba 52 zilizokuwa wakiishi wananchi zilivunjwa huku nyingine 10  zikiwa katika hatua ya kuvunjwa ili kutoa nafasi zaidi ya kuendeleza ujenzi huo, wakati ambapo Serikali tayari imeshalipa fedha  kuwawezesha wamiliki kukodi sehemu nyingine na kufidia usumbufu wa kuhama.
Alieleza kuwa baada ya hatua za ujenzi kukamilika wananchi hao watarudi eneo hilo na kupatiwa nyumba mpya bila malipo ya ziada.
Aliushukuru Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) kwa kukubali kuikopesha Serikali shilingi Bilioni 20 ili ziweze kutumika kuambatana na mahitaji ya mradi yatavyojitokeza.
Aidha, aliwashukuru wananchi wa Kwahani kwa uzalendo na kuwa mstari wa mbele kushirikiana na Serikali kufanikisha ujenzi wa makaazi mapya.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2TazqY4
via

Post a Comment

0 Comments