Ticker

10/recent/ticker-posts

FLAVIANA MATATA AONGOZA WANAMITINDO WENZAKE KUTEMBELEA HIFADHI YA SERENGETI

MWANAMITINDO maarufu Duniani Mtanzania anayefanya shughuli zake nchini Marekani,Flaviana Matata ametembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kujionea vivutio mbalimbali vya kitalii akiwa ameambatana na Wanamitindo wenzake kutoka Marekani.

Flaviana Matata  ameongozana na wanamitindo hao akiwemo: Shelby Colemans, Daniella Evans na Awa Florence Mafany ambao kila mmoja anafanya shughuli za mitindo huku wakiwa na wafuasi wengi kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii.

Flaviana Matata akiwa na rafiki zake hao, wameweza kushuhudia vivutio vya utalii ndani ya Serengeti ikiwemo wanyama mbalimbali sambamba na uzuri wa Hifadhi hiyo ambayo ni kubwa hapa Nchini.

Ziara hiyo ya kuambatana na Wanamitindo hao ni kwa lengo la kuona vivutio vya utalii vilivyoko katika hifadhi na kuvitangaza.



 


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2RcdgSL
via

Post a Comment

0 Comments