Ticker

10/recent/ticker-posts

Wanafunzi 81 St. Anne Marie wachaguliwa shule za vipaji maalum

WANAFUNZI 81 waliomaliza darasa la saba katika shule ya St. Anne Marie Academy ya Mbezi Kimara wamechaguliwa kujiunga na shule za serikali za wanafunzi wenye vipaji maalum.

Akizungumza na Michuzi media, Mkuu wa shule hiyo, Gradius Ndyetabula amesema jumla ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kumaliza darasa la saba mwaka huu walikuwa 99 amapo katika matokeao yao anafunzi wote 99 wa shule hiyo walifaulu kwa wastani wa daraja A na shule hiyo kushika nafasi ya kwanza katika Wilaya ya Ubungo, ya kwanza Mkoa wa Dar es Saam na ya 13 kitaifa.

Amesema shule hiyo pia kwenye matokeo ya darasa la saba mwaka jana wanafunzi wote walifaulu kwa wastani wa alama A na shule ikashika nafasi ya kwanza wilaya ya Ubungo, nafasi ya kwanza Mkoa wa Dar es Salaam na nafasi ya sita kitaifa.

Amesema siri ya mafanikio hayo ni maandalizi mazuri ya wanafunzi hao hivyo kuchaguliwa kwao kwenda kwenye shule za vipaji maalum si jambo la kubahatisha.

“Shule hii inautajiri wa miundombinu ambao unatokana na uzoefu wa muda mrefu kwani shule hii imetimiza miaka 20 tangu ianze kutoa wanafunzi katika mitihani ya kitaifa, kutokana na mafanikio haya tunawaomba wazazi waendelee kutuamini na kutuletea watoto na mwezi huu wa Desemba tunaendelea kupokea wanafunzi kwa mwaka mpya wa masomo,” alisema

Ndyetabula amesema kwa upande wa sekondari shule ya St Anne Marie Academy matokeo yamekuwa mazuri kwani matokeo ya kitaifa kidato cha nne 2018, wanafunzi 28 walipata DIV One, wanafunzi 58 DIV II na wanafunzi 48 DIV III na hakuna mwanafunzi aliyepata daraja la nne wala 0.

"Kwenye matokeo ya kidato cha sita 2019 wanafunzi 19 walipata DIV one, wanafunzi 47 DIV II, wanafunzi 21 DIV III na kwamba hakuna mwanafunzi aliyepata daraja la nne wala 0 kwenye matokeo hayo...,

“Namshukuru mwalimu mkuu na timu yake kwa umahiri walioonyesha kuwaandaa vijana hawa, miundombinu bora yote ipo kuanzia maabara, maktaba, maji na umeme wa uhakika maana maji hata yakikatika tunaakiba ya mwezi mzima, umeme vile vile hatuna shida hapa ni kusoma tu ” amesema Mkurugenzi wa shule hizo, Dk. Jasson Rweikiza

“Tunawashukuru wazazi kwa kutuamini na tunawaomba muendelee kutuamini kwa kutupa watoto wenu tumekuwa tukiendelea kuboresha mazingira ya kujisomea mwaka hadi mwaka,” alisema
Mkuu wa Taaluma Msaidizi wa St Anne Marie Academy, Kasenga James (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Shule hiyo, Gradius Ndyetabula baada ya wanafunzi 81 wa shule hiyo waliomaliza darasa la saba kuchaguliwa kujiunga na shule za vipaji maalum hivi karibuni.




from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2YxHCmc
via

Post a Comment

0 Comments