Ticker

10/recent/ticker-posts

WAKUU WAWILAYA ZOTE ZA MKOA WA ARUSHA KUSANYENI DATA ZA WAZAZI WASIOWEZA KUTIMIZA WAJIBU-GAMBO


Na Woinde Shizza, Arusha

Mkuu wa mkoa Wa Arusha Mrisho Gambo amewataka wakuu Wa wilaya zote za mkoa Wa Arusha kukusanya data za wazazi ambao wameshidwa kutimiza wajibu wao Wa kuwasomesha pamoja na kuwahudumia watoto wao ambao wapo chini ya miaka 18.

Aidha pia aliwataka wapeleke taarifa zote za matukio ya ambayo yameripotiwa kwenye wilaya zao yanaohusiana na ukatili Wa kijinsia klikiwemo idadi ya mashauri yaliopelekwa mahakamani , mangapi hayajapelekwa mahakamani ,na sababu ya kutopeleka ninini kama kunavikwazo waviainishe ili viweze kufanyiwa Kazi haraka iwezekanavyo.

Aliyasema hayo Jana kwenye kilele cha maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili Wa kijinsia kwa mkoa Wa Arusha yaliongozwa na maandamano ya jeshi LA Polisi na kuhitimishwa katika hospital ya rufaa ya mkoa Wa Arusha (mount Meru) ambayo yamebeba kauli mbiu ya "Kizazi chenye usawa simama dhidi ya ubakaji".

" tutachukuwa taarifa zote tutakazo zibaini na tutachunguza kama changamoto zipo katika mahakamani zetu , Polisi , au kwa wataalamu wetu Wa afya ambao wanatakiwa kutoa taarifa rasmi ya ripoti ya kitaalamu yakuthibitisha kama kweli kuna MTU amefanyiwa ukatili Wa kijinsia ili iwe kama ushaidi Wa kumpeleka muhalifu mahakamani tukiwa na ushaidi Wa kutosha na tunasema Leo sisi kama mkoa Wa Arusha tumeanza Kazi ya kuwasaka na kuwachukulia watu wale wote wanaofanya matukio ukatili Wa kijinsia"alisema Gambo

Alibainisha kuwa taarifa inaonyesha kadri Siku sinavyoenda matukio ya ukatili Wa kijinsia yanapungua lakini taarifa,mwitikio na twasira inaonyesha matukio ya ukatili Wa kijinsia yapo ,na hii inatokana uwezekano Wa baadhi ya matukio kutoripotiwa katika sehemu husika au baadhi ya wananchi wamekata tamaa baada ya kuona matukio wanayoripoti hayafiki katika hatua ambayo waowanategemea.

Kwa upande wake kamanda Wa Polisi mkoa Wa Arusha Jonathan Shana alisema wao kama kama jeshi LA Polisi wameshaanza Kazi rasmi ya kuwathibiti watu wanaofanya matendo ya ukatili Wa kijinsia nawanaanza rasmi kuwasaka popote pale walipo na watawachukulia hatua Kali za kisheria hivyo aliwasihi wananchi watii sheria bila shuruti , na kuwaambia kuwa mapambano ya kupinga ukatili Wa kijinsia ni wakila mtu awe mwanaume au mwanamke.

Nae mganga mfawithi Wa hospital ya rufaa ya mount Meru Shafii Msechu alisema kuwa kwa mwaka huu wamepokea waanga Waliofanyiwa ukatili Wa kijinsia 333 waliopelekwa mahakamani 10 kesi zilizopelekwa mahakamani zikiwa ni tisa na wanahakisha wahalifu wanachukuliwa hatua ,alisema wananchi wamekuwa hajitokezi kutoa taarifa za namna wanavyofanyiwa ukatili huo wengi wao wakiwa wanaogopa kuonekana kitu ambacho kinawanyima haki yao.

Nae kamishina msaidizi Wa Polisi ambae pia ni Mwenyekiti Wa mtandao Wa Polisi wanawake mkoa Wa Arusha (TPF-NET) Mary Kipesha alisema kuwa matukio ya ukatili Wa kijinsia yamepungua sana kwa mwaka huu tofauti na mwaka Jana ambapo Kwa kipindi cha mwaka 2018 kesi za ukatili Wa kijinsia ziliripotiwa 161 huku mwaka huu 2019 January hadi December zikiwa zimeripotiwa kesi 89 ambapo kunaupungufu Wa asilimia 32.5%.

Kwa upande Wa kesi za kulawiti mwaka Jana 2018 zilikuwa 62 huku mwaka huu 2019 kwa kipindi cha January adi December zikiwa na kesi 52 ambapo kunaupungufu Wa asilimia 7.9% na hii inaonyesha wamepata mafanikio makubwa mno ya kupunguza uhalifu Wa unyanyasaji Wa kijinsia , hivyo katika kuakikisha swala hili linaisha wataendelea kutoa Elimu kwa wanafunzi Wa mashuleni, vyuoni pamoja na wananchi kwa ujumla .


Mkuu Wa mkoa Wa Arusha akiongea katika kilele cha siku 16 cha maadhimisho ya wiki ya upingaji wa ukatili wa kijinsia kwa watoto
kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Jonathan Shana akiongea wakati kilele cha siku 16 za maadhimisho kupinga vita ukatili Wa kijinsia kwa watoto

Kamishina msaidizi wa Polisi ambae pia ni Mwenyekiti Wa mtandao Wa Polisi wanawake mkoa Wa Arusha (TPF-NET) Mary Kipesha akisoma risala mbele ya mgeni rasmi.


Askari wa jeshi lA Polisi mkoa wa Arusha wakiwa katika maandamano


Mkuu wa. Mkoa Wa Arusha wakiwa ananyakua nyakua na askari Polisi Wa mkoa Wa Arusha Mara baada ya maandamano kuwasili ndani ya hospital ya rufaa ya Mount Meru


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2PGsXRm
via

Post a Comment

0 Comments