Ticker

10/recent/ticker-posts

WAJUMBE BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA ARUSHA DC WAWANYOOSHEA KIDOLE BAADHI YA WAFANYAKAZI WAZEMBE UKUSANAYAJI MAPATO


ALAMIKIA UKUSANYAJI HAFIFU MAPATO 

Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha

WAJUMBE kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Arusha DC wamesema uzembe wa  ukasanyaji mapato  kwa baadhi ya wafanyakazi wa halmashauri hiyo umekuwa moja ya sababu ya kutofikia malengo ya makadirio ya makusanyo kwa mwaka .
 
Hayo yamezungumzwa leo katika kikao  cha baraza la madiwani  wakati wa kikao cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji Wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Julai -September 2019 kilichofanyika katika ukumbi Wa halmashauri hiyo.

Akizungumza katika kikao hicho  Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Baraka Simon amesema kuwa baadhi ya wafanyakazi wamekuwa hawafanyi kazi vizuri ya ukusanuaji wa mapato  na wamekuwa hawafatilii  wakandarasi waliopewa zabuni za kukusanya mapato hali  inayoikosesha halmashauri fedha zamapato,hivyo kuifanya hata halmashauri kushidwa kulipa baadhi ya madeni ambayo wanadaiwa.

"Changamoto ya mapato ni kubwa mno kwani hata hawa  wakandarasi waliopewa zabuni za kukisanya ushuru mbalimbali wamekuwa hawazileti kama ipasavyo  hali inayofanya halmashauri tukose mapato , na mapato yetu kushuka ,"amesema.

Ameongeza wameweza kubaini baadhi ya changamoto ambazo zinasababisha mapato hayo kushuka  ,ambapo kwa asilimia kubwa sana ni pamoja na uvivu wa baadhi ya wataalamu wao wa halmashauri hiyo ambapo katika kutatua  hilo wao kama baraza la  madiwani  wametoa maelekezo  kuhakikisha ,ukusanyaji mapato unaongezeka.

Kwa upande wake Wa Diwani Wa kata ya Ilikiding'a Loth Mungaya  alisema kuwa halmashauri hiyo inavyanzo   vyanzo vingi vya mapato ikiwemo ,machimbo ya moramu  ,maegesho ya magari,pamoja na mchanga na kwa upande wa mchanga  na Moramu watu wamekuwa wanachota usiku na mchana lakini wanashangaa kuona halmashauri  haiingizi mapato na ikiendelea hivi  itapelekea halmashauri kushidwa kujiendesha na mwishowe kufutwa kabisa.

Akizungumzia suala hilo Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Arusha Dc Alvera Ndabagoye amesema atafanyia kazi na iwapo atabaini mfanyakazi yeyote anajinufaisha na fedha za mapato ya halmashauri atachukuliwa hatua kali ikiwemo na kufukuzwa kazi.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha,Alvera Ndabagoye akijibu maswali yaliyoulizwa na madiwani Wa halmashauri hiyo katika kikao cha madiwani wakati Wa kikao cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji Wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Julai -September 2019.(picha na Woinde Shizza, Arusha ).

Mwenyekiti Wa halmashauri ya Arusha Baraka Simon  akiongea katika kikao cha kawaida cha  madiwani cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji Wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Julai -September 2019



from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2s2ADp9
via

Post a Comment

0 Comments