ALAMIKIA UKUSANYAJI HAFIFU MAPATO
Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha
WAJUMBE kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Arusha DC wamesema uzembe wa ukasanyaji mapato kwa baadhi ya wafanyakazi wa halmashauri hiyo umekuwa moja ya sababu ya kutofikia malengo ya makadirio ya makusanyo kwa mwaka .
Hayo yamezungumzwa leo katika kikao cha baraza la madiwani wakati wa kikao cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji Wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Julai -September 2019 kilichofanyika katika ukumbi Wa halmashauri hiyo.
Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Baraka Simon amesema kuwa baadhi ya wafanyakazi wamekuwa hawafanyi kazi vizuri ya ukusanuaji wa mapato na wamekuwa hawafatilii wakandarasi waliopewa zabuni za kukusanya mapato hali inayoikosesha halmashauri fedha zamapato,hivyo kuifanya hata halmashauri kushidwa kulipa baadhi ya madeni ambayo wanadaiwa.
"Changamoto ya mapato ni kubwa mno kwani hata hawa wakandarasi waliopewa zabuni za kukisanya ushuru mbalimbali wamekuwa hawazileti kama ipasavyo hali inayofanya halmashauri tukose mapato , na mapato yetu kushuka ,"amesema.
Ameongeza wameweza kubaini baadhi ya changamoto ambazo zinasababisha mapato hayo kushuka ,ambapo kwa asilimia kubwa sana ni pamoja na uvivu wa baadhi ya wataalamu wao wa halmashauri hiyo ambapo katika kutatua hilo wao kama baraza la madiwani wametoa maelekezo kuhakikisha ,ukusanyaji mapato unaongezeka.
Kwa upande wake Wa Diwani Wa kata ya Ilikiding'a Loth Mungaya alisema kuwa halmashauri hiyo inavyanzo vyanzo vingi vya mapato ikiwemo ,machimbo ya moramu ,maegesho ya magari,pamoja na mchanga na kwa upande wa mchanga na Moramu watu wamekuwa wanachota usiku na mchana lakini wanashangaa kuona halmashauri haiingizi mapato na ikiendelea hivi itapelekea halmashauri kushidwa kujiendesha na mwishowe kufutwa kabisa.
Akizungumzia suala hilo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha Dc Alvera Ndabagoye amesema atafanyia kazi na iwapo atabaini mfanyakazi yeyote anajinufaisha na fedha za mapato ya halmashauri atachukuliwa hatua kali ikiwemo na kufukuzwa kazi.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha,Alvera Ndabagoye akijibu maswali yaliyoulizwa na madiwani Wa halmashauri hiyo katika kikao cha madiwani wakati Wa kikao cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji Wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Julai -September 2019.(picha na Woinde Shizza, Arusha ).
Mwenyekiti Wa halmashauri ya Arusha Baraka Simon akiongea katika kikao cha kawaida cha madiwani cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji Wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha robo ya kwanza ya Julai -September 2019
from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2s2ADp9
via
0 Comments