Ticker

10/recent/ticker-posts

VIJIJI 4 VYAKOSA MAWASILIANO SIKU KADHAA KATA YA ENGARUKA.

Na.Vero Ignatus,MONDULI

Zaidi ya hekari 200 za mazao mchanganyiko zimeharibiwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika kijiji cha Mbaash kata ya Selela wilaya ya monduli Mkoani Arusha.

Ambapo alisema kuwa katika eneo hilo niwakulima mbalimbali wanalima eneo la zaidi ya hekari 480 zilizoko ktika kijij hicho ambapo kwa sasa sehemu kubwa la eneo hilo limezingirwa na maji hali ambayo imewaweka katika njia panda wakulima wa eneo hilo.

Hayo yameelezwa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Monduli  ambae ni Mkuu wa Wilaya hiyo IDD Hassan Kimanta mara baada ya kutembelea  baadhi ya maeneo ambayo mvua imeathiri katika kata ya Selela iliyoko wilayan Monduli mkoani Arusha.

Hata hivyo amesema kuwa wametembelea eneo hilo kuangalia na kutathimi hali halisi ya uharibifu wa mazao hayo ya chakula katika eneo hilo na kuweza kuchukua jitihada za dharura ili kuweza kunusuru mazao hayo ya wakulima ili kuepuka kupata hasara zaidi katika eneo liliobaki katika hekari hizo ili pia waakulima wa eneo hilo kutoendelea kupata hasara ili kuweza kutafutia njia ya kuchepusha maji hayo kuepuka hasara kubwa kwa wakulima hao na mvua ambazo zinaenedela kunyesha hasa kipidi hiki.

Amelezea na  kubainisha jitihada zinazoendelea kufanyika ikiwemo za kuweka vifusi katika baadhi ya maeneo ili kuunganisha mawasiliano wakati jitihada nyingine zikifanyika.

Amesema kuwa mvua hizo zinzoendelea kunyesha mkoani hapa zimeleta uharibifu mkubwa sana ikiwemo imeharibu Miundo mbinu ya Barabara, ambayo ndio kiungo kikuu cha Mawasiliano vya Kutoka Loliondo kuja Jijini Arusha.

Kwa upande wake kaimu meneja wa Tarura kutoka halmashauri ya Monduli alisema kuwa Mhandisi Janeth Erasto Mhokera amesema kuwa kufatia mvua hizo ambazo zimeleta uharibifu mkubwa kwa kukosekana kwa mawasiliano kama Tarura wamefanya jitihada za makusudi ii kuweza kurejesha mawasiliano ya vijiji hivyo ,pamoja na wakulima hao kuweza kuchepusha maji hayo ili kuweza kunusuru hekari nyingine kuendelea kuharibika na pia wakandrasi wako site kuendelea kumarisha barabara zote katika wilaya ili kuweza kukabiliana na hali ya mvua ambazo zinaendelea kunyesha karibia maeneo mbalimbali mkoani hapa.

Nae mtendaji wa kijiji wa kata ya Selela  bwana Emmanueli Nitalani   alisema kuwa kwasasa hali ya uharibifu wa mazao hayo mchanganyiko nikubwa sana  kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani hapa hasa kata hiyo karibia eneo kubwa la hekari 200 zimezingirwa na maji mengi haliambayo imewaweka njia panda na sintofahamu ya kujua cha kufanya katika eneo hilo walilolima hasa mahindi hasa kipindi hiki cha msimu wakilimo.

Kwa upande wake Wakulima wa eneo hilo bibie  Elikaa na Moleli laizer kutoka kata ya engaruka wa maeneo haya wanasema mbali na Miundombinu ya barabara pia Mvua iliyonyesha kwa imesababisha hekari za mazao yao shambani kuharibika kutokana na kusombwa na Mafuriko hali mbayo inawarudisha nyuma katika jitihada za kuweza kujikwamua katika lindi la umaskini.

Wakulim hao wameiomba Serikali kuweza kuwaletea mahindi kwa bei nafuu na kuweza kuwasaidia namna bora ya kuweza kunusuru mazao yao waliyolima eneo hilo .

hizo pia wameiomba serikali kuwza kuwapatia mbegu ili waweze kurudia na kuwahi hasa msimu huu wa mvua ili kutoweza kupata cahakula kingi kutokanana hali ambayo imekumba Kijiji cha Mbaash  katika kata ya Selela.
 Picha ni Mkuu wa wilaya ya monduli  Idd Kimanta akiwa wajumbe(hawapo pichani) wa Kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya ya  Monduli mkoa wa Arusha wakikagua moja eneo la daraja katika kata ya Engaruka .



from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2temJAO
via

Post a Comment

0 Comments