Ticker

10/recent/ticker-posts

SHEREHE ZA UHURU ZAWAKUTANISHA TENA FREEMAN MBOWE, SUMAYE NA LOWASSA


Na Said Mwishehe,Michuzi Globu-Mwanza

WAMEKUTANA katika Sherehe za uhuru za miaka 58 za uhuru! Ndivyo unavyoweza kuelezea baada ya Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe kukutana na aliyekuwa Mgombea urais wa Chama hicho katika uchaguzi mkuu mwaka 2015 Edward Lowassa. Mbali ya kukutana na Lowassa, Mbowe pia amekutana na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani na Waziri Mkuu wa zamani Frederick Sumaye ambaye naye siku za karibuni ametangaza kujindoa ndani ya chama hicho.

Kupitia sherehe hizo za Uhuru viongozi hao wamekutana ana kwa ana ndani ya Uwanja wa CCM Kirumba ambako ndiko zimefanyika sherehe hizo zikiongozwa na Rais Dk.John Magufuli.

Iko hivi Mbowe aliingia uwanjani hapo akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati Lazaro Nyalandu ambao kila mmoja alikuwa amevalia suti nadhifu na mashati meupe ndani.Safarii hii hawakuwa wamevalia sare zao za kombati.

Katika uwanja huo uwanja hakukuwa na wanachama wa Chadema waliovaa sare za chama hicho.Miaka ya nyuma ilizoeleka kwenye sherehe za kitaifa wana-Chadema kuvalia sare zao lakini safarii hiii wameamua kuweka kando. Wakati wa wana CCM baadhi yao wao walionekana wakiwa na mavazi yao maalumu yenye chama za rangi za chama hicho za kijani na njano.

Hata hivyo Mbowe na Nyalandu baada ya kuingia katika uwanja huo mapema asubuhi waliingia kwa kupita katika lango la viongozi wa kitaifa na kupokelewa kwa heshima zote kama ilivyofanyika kwa viongozi wengine.

Walipopokelewa walioneshwa eneo maalumu ambalo lilitengwa kwa ajili ya wageni wa kitaifa kuungana na viongozi wengine ambao tayari walikuwa wamefika eneo hilo la uwanja wa CCM Kirumba.

Kwa kukumbusha tu Mbowe na Chama chake cha Chadema walikuwa wamesusia sherehe hizo kwa miaka mitatu mfululizo kuanzia mwaka 2015 baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani.

Hata hivyo wakati Mbowe anazungumza mbele ya Rais Dk.Magufuli alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa ameamua kushiriki kwenye sherehe hizo yeye na Chama chake kama inshara ya kurejesha umoja , upendo na msikamano kwa Watanzania.

Ambapo ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa Rais Magufuli kuhakikisha anarejesha utengamano wa maeleno na maridhiano huku pia akiomba uhuru wa demokrasia.



from MICHUZI BLOG https://ift.tt/345iVi2
via

Post a Comment

0 Comments