Ticker

10/recent/ticker-posts

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA DARAJA LA KIGONGO-BUSISI LINALOUNGANISHA WILAYA YA MISUNGWI NA SENGEREMA MKOANI MWANZA

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisogea kuangalia picha ya mfano wa Daraja hilo litakalojengwa kutokea Kigongo Misungwi hadi Busisi Sengerema mkoani Mwanza. Daraja hilo litakalopita ziwani litakuwa na urefu wa km 3.2 na kufanya kuwa Daraja refu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki. 

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti walipokuwa wakiangalia picha ya mfano wa Daraja hilo litakalojengwa kutokea Kigongo Misungwi hadi Busisi Sengerema mkoani Mwanza. Daraja hilo litakalopita ziwani litakuwa na urefu wa km 3.2 na kufanya kuwa Daraja refu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki. 

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na viongozi wengine akivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi wa Daraja la kutoka Kigongo hadi Busisi lenye urefu wa km 3.2 katika sherehe zilizofanyika katika eneo la Kigongo Misungwi mkoani Mwanza.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli watatu kutoka kulia pamoja na baadhi ya Viongozi Wakuu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mitambo itakayotumika katika ujenzi wa Daraja hilo refu kupita yote katika ukanda wa Afrika Mashariki lenye urefu wa km 3.2 katika sherehe zilizofanyika katika eneo la Kigongo Misungwi mkoani Mwanza.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia picha ya mfano wa Daraja hilo litakalojengwa kutokea Kigongo Misungwi hadi Busisi Sengerema mkoani Mwanza. Daraja hilo litakalopita ziwani litakuwa na urefu wa km 3.2 na kufanya kuwa Daraja refu katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma mara baada ya kuweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa Daraja la kutoka Kigongo hadi Busisi Misungwi mkoani Mwanza.

 Mbunge wa Misungwi Mhe. Charles Kitwanga akicheza ngoma ya Gobogobo wakati wa sherehe ya uwekaji wa  jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa Daraja la kutoka Kigongo hadi Busisi Misungwi mkoani Mwanza.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza wakati akiwa na Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Iseni B Salma Yasin ambaye alielezea vizuri kero mbalimbali za Shule yao na kufanikiwa kuchangiwa kiasi cha Shilingi milioni 5 na Mhe. Rais Dkt. Magufuli. PICHA NA IKULU






from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2ro2aBk
via

Post a Comment

0 Comments