Ticker

10/recent/ticker-posts

NEWS ALERT : WATU ZAIDI YA 37 WALAZWA HOSPITALI YA RUFAA DODOMA WAKIDAIWA KULA CHAKULA CHENYE SUMU MSIBANI

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe Patrobas Katambi akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma ambao wamelazwa kwa kile kinachoelezwa kula chakula chenye sumu.


 Watu zaidi ya 37 wamelazwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma (General Hospital)  kwa ugonjwa wa kuhara na kutapika baada ya kula chakula kinachosadikiwa kuwa na sumu kwenye msiba eneo la Mtumba nje kidogo ya Jiji la Dodoma.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Patrobas Katambi tayari kashafika hospitalini hapo na amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.


TUTAWALETEA TAARIFA ZAIDI KUHUSU TUKIO HILI KADIRI YA ZITAKAVYOPATIKANA.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/34m53jt
via

Post a Comment

0 Comments