Ticker

10/recent/ticker-posts

MNYIKA, LEMA NDANI YA MAGANDWA,CCM KIJANI NA NJANO YAO WAKATI WA SHEREHE ZA UHURU


Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Mwanza

MBUNGE wa Kibamba jijini Dar es Salaam John Mnyika pamoja na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema wakiwa wameongozana na Meya wa Ubungo Boniface Jacob wametinga uwanja wa CCM Kirumba Mjini Mwanza katika Sherehe ya miaka 58 ya Uhuru wakiwa wamevaa sare zao za magwanda huku wana CCM wakiwa na sare zao za kijani na njano.

Wabunge hao kama ambavyo ilivyo kwa viongozi wengine wa kisiasa walioshiriki sherehe hizo walipata nafasi ya kukaa jukwaa kuu kushuhudia kila kinachoendelea uwanjani hapo.Viongozi wa Chadema kwa muda mrefu walikuwa wamesusia kushiriki sherehe hizo lakini safari hii wameona isiwe tabu. Mbunge wa zamani wa Jimbo la Nyamagana naye alikuwa miongoni mwa walioshiriki.

Wakati huo huo mbali ya wabunge hao, pamoja na wabunge wengine lukuki wa CCM walioshiriki katika sherehe hiyo, idadi kubwa ya wananchi wa Jiji la Mwanza na mikoa jirani nao wamejitokeza kwa wingi,Idadi ya watu ilikuwa kubwa kiasi cha Rais Dk.John Magufuli kueleza watu waliojitokeza ni wengi sana na haijapata kutokea kuona kuna viongozi wa kada zote na kwa awamu tofauti.

Ukweli ni kwamba hamasa ya wananchi wa Mwanza kushiriki kwenye sherehe hizo ni kubwa na mapema kabisa ilionekana namna ambavyo makundi ya watu yalivyokuwa yakipita mtaani kuelekea CCM Kirumba.

Katika kuhakikisha watu wanapata nafasi ya kuingia uwanjani mapema, milango ilikuwa imefunguliwa saa 10 alfajiri na hivyo kutoa nafasi kwa kila aliyekwenda kutotumia muda mwingi kupanga foleni ya kuingia uwanjani hapo.

Ilpofika saa moja asubuhi karibu majukwaa yote ya uwanjani hapo yalikuwa yamejaa na wakati huo huo watu wakiendelea kuingia kwa kupanga foleni.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella, alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa idadi kubwa ya watu kujitokeza uwanjani hapo ni mapenzi ya Watanzania kwa Serikali na Taifa lao.
MBUNGE wa Kibamba jijini Dar es Salaam John Mnyika


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2s5lF1v
via

Post a Comment

0 Comments