Ticker

10/recent/ticker-posts

Kishindo cha Funga mwaka’ ya Tigo yaendelea kutoa Zawadi

Mshindi wa 5m/- wa promosheni ya Kishindo cha Funga mwaka Emmanuel Mwaijumba akipokea mfano wa hundi kutoka kwa balozi wa kampeni hiyo Meena Ally jijini Dar es Salaam. 

Dar es Salaam. Emmanuel Mwaijumba, ambaye ni mkazi wa Mikocheni, Dar es Salaam amejinyakulia zawadi ya Sh Milioni 5 kupitia kampeni ya ‘Kishindo cha Funga Mwaka’ inayofanywa na Kampuni ya Mawasiliano Tigo. 

Kwa kupitia kampeni hiyo, mkuu wa kitengo cha bidhaa cha Tigo Pesa, James Sumari amesema kampuni yao imetenga zawadi zenye thamani ya Sh Milioni 500 kwa wateja 331 nchi nzima wanaoweka na kupokea pesa kwenye akaunti zao za Tigo Pesa. 

Ili kushiriki alisema, mteja wa tigo pesa anatakiwa kuweka miamala inayoanzia Sh 10,000 kwenye akaunti yake ya Tigo Pesa kupitia kampeni hiyo maalumu kwa ajili ya msimu huu wa kufunga mwaka itakayodumu kwa mwezi mmoja. 

“Wateja wanatakiwa kuweka pesa kwa Wakala au kupokea pesa kwenye akaunti zao za Tigo, Pesa kutoka benki, mitandao mingine au vyanzo vingine mbalimbali na moja kwa moja watakuwa kwenye nafasi ya kushinda,” alisema. 

Alisema kwa kupitia kampeni hiyo kutakuwa na washindi watatu wa mwezi watakaoibuka na zawadi ya Sh Milioni 20 kwa mshindi wa kwanza, Sh Milioni 15 wa pili na Sh Milioni 10 wa tatu huku kila wiki ikitoa washindi nane wa Sh Milioni 5 kila mmoja na wengine nane wa Sh Milioni moja kila siku. 

Akishuruku kwa zawadi hiyo, Mwaijumba ambaye ni mfanyabiashara alisema atatumia kiasi hicho cha kukuza biashara yake ili kipato atakachopata kutokana na mauzo atakayokuwa akiyafanya kisaidie kuchangia kipato cha familia na kulipia ada za shule 

Mpaka sasa promosheni imeshawazawadia washindi zaidi ya 20 wa wiki, na zaidi ya 120 wa kila siku.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/35Qxck8
via

Post a Comment

0 Comments