Ticker

10/recent/ticker-posts

KATIBU MKUU MAMBO YA NJE AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA CHINA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (kushoto) akisaini kitabu cha Wageni alipokutana kwa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Chen Xiaoding (kulia) jijini Beijing, China Desemba 11, 2019. Dkt. Mnyepe yupo nchini humo kushiriki Mkutano wa Pili wa Jukwaa la Haki za Binadamu kwa Nchi zinazoendelea.

Dkt. Mnyepe amemuhakikishia Mhe. Chen kuwa, Tanzania itaendelea kudumisha ushirikiano na China kupitia Jukwa la Ushirikiano kati ya Afrika na China (Forum on China-Africa Cooperation - FOCAC). Aidha, kwa pamoja wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha kuwa, mageuzi ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yanakuwa na tija kwa chi zinazoendelea hususan nchi za Afrika.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (kushoto) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Chen Xiaoding wakiwa katika picha ya pamoja jijini Beijing, China.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China Mhe. Chen Xiaoding walipokutana kwa mazungumzo jijini Beijing, China Desemba 11, 2019


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2RKzuxg
via

Post a Comment

0 Comments