Ticker

10/recent/ticker-posts

DCB YAZINDUA MKOPO WA ADA YA SHULE

Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya Biashara ya DCB, James Ngaluko (wa pili kulia), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma ya mkopo maalumu wa ada ya shule jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni Balozi wa DCB Skonga, Zamaradi Mketema, Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa DCB, Rahma Ngassa na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Fortunata Benedict.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Biashara ya DCB, Fortunata Benedict (kulia), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma ya mkopo maalumu wa ada ya shule jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa DCB, Rahma Ngassa na Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, James Ngaluko. 
Balozi wa bidhaa ya DCB Skonga ya Benki ya Biashara ya DCB, Zamaradi Mketema (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma ya mkopo maalumu wa ada ya shule jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni, Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa DCB, Rahma Ngassa, Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, James Ngaluko na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Fortunata Benedict.

=====  =======  ======  ========  ========
 BENKI ya Biashara ya DCB imezindua huduma ya mkopo maalumu wa Ada ya Shule ikiwa ni fursa nyingine tena itakayowawezesha wateja wa benki hiyo kulipa ada za watoto wao kwa wakati na uhakika.

Mkopo wa ada wa DCB ni mwendelezo wa mkakati wa benki kubuni huduma na bidhaa bora zinazowanufaisha wateja. Benki imekuja na bidhaa hii ya mkopo wa ada katika harakati ya kuwaondolea hofu wazazi linapokuja suala zima la elimu kwa watoto wao hii ni sambamba na akaunti ya DCB Skonga inayomuwezesha mtoto kusomeshwa pindi mzazi anapopata ulemavu wa kudumu ama kifo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi rasmi wa mkopo huu, Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano Bi Rahma Ngassa alisema ‘’DCB inaendelea kuleta kwenye soko bidhaa zinazo kidhi maisha ya watanzania, benki hii ni ya watanzania hivo ni lazima kuja na fursa inayowawezesha wateja wetu kunufaika na benki yao.

Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, Bwana James Ngaluko aliongeza ‘’mkopo huu ni wa dharura na ni suluhisho kubwa kwa wateja wetu, siku hazilingani na kama Benki tunataka watoto wetu wasome, elimu ndio ufunguo wa maisha hivyo tunampa mzazi fursa ya kupata mkopo wa dharura ndani ya masaa 48 kwa ajili ya ada ya mtoto pindi amekwama.

Alisema wakati tunaendelea kusherekea sikukuu za mwisho wa mwaka na kukaribisha mwaka 2020, Benki tumeona tuwazawadie zawadi ya kipekee kabisa wateja wetu kwani ni jambo lililo dhahiri kuwa suala la ada ni moja ya changamoto kubwa inayowakabili wazazi wengi kila ifikapo mwanzoni mwa mwaka. Mkopo wa Ada wa DCB una riba ya chini sana na utalipwa moja kwa moja kwenye shule ya mtoto. Mkopo huu unakupa fursa ya kukopa hadi shilingi milioni tano ndani ya masaa 48 na muda wa marejesho unachagua mwenyewe hadi miezi sita.

Nae Mkuu wa kitengo cha Wateja Binafsi Bi Fortunata Benedict alisema ‘’Wazazi wengi kwa kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto wao wamejikuta wakihangaika kutafuta fedha za ada kwa njia zozote hivyo kujikuta kuingia katika matatizo. Mzazi sasa huna haja ya kupata stress za kulipa ada, acha DCB ikufikirie masuala ya elimu ya mtoto wako hii ni suluhisho la uhakika la kifedha. 


Ikumbukwe kua mwaka wa 2019 DCB imetoa fursa mbalimbali kwa wateja ikiwemo

· DCB imewapa maelfu ya watanzania fursa ya kuwekeza kwa kununua Hisa na kua wamiliki halali wa benki hii kupitia mfumo wa hisa za upendeleo

· DCB kibubu inampa fursa mteja kuweka akiba mwenyewe kidogo kidogo kupitia simu ya mkononi (DCB Digital) na kuhakikisha watanzania wengi wanafikiwa na huduma za kibenki.

· DCB ilizindua DCB Sokoni inayolenga kumkomboa mkulima na mfanyabiashara wa kilimo katika mnyororo wa thamani

· DCB Lamba kwanza inayomuwezesha mteja kupata riba ya hadi asilimia 14% papo hapo na kila mwanzo wa mwezi.

· DCB Skonga, ikilenga kuwasaidia wazazi katika suala zima la elimu ya watoto wao pindi watakapopata majanga ya ulemavu wa kudumu au kifo.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2s1i1WN
via

Post a Comment

0 Comments