Ticker

10/recent/ticker-posts

BRELA YAFANYA BONANZA LA MICHEZO KWA ZAIDI YA VIKUNDI 48 JIJINI DAR ES SALAAM

Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF Anna Makinda ambaye alikuwa mgeni rasmi katika bonanza la Brela akikagua timu ya mpira wa miguu iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF Anna Makinda (katikati) akiwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Loy Watson Mhando ( wa kwanza kushoto) wakifuatilia bonanza la michezo lililoandaliwa na BRELA jijini Dar es Salaam.
---
Katika kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) wamefanya bonanza la michezo kwa vikundi 48 vya mpira wa miguu likiwa na lengo wa kujenga afya na kuimarisha uhusiano baina ya wafanyabiashara.
Bonanza hilo lilofanyika pia lilikuwa na lengo la kuwaelezea umuhimu wa bima ya afya kwa dereva wa bodaboda na wananchi kwa ujumla.
Akizungumza Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Bi. Loy Watson Mhando amesema kuwa wamefurahishwa na jinsi watu walivyojitokeza kushiriki mazoezi na kupima afya zao jambo linalisaidia kupunguza wagonjwa.
Bonanza hilo lilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF Anna Makinda (katikati) ambaye alikuwa mgeni rasmi limefanikiwa kwa asilimi 100 kwa kuweza kufikisha malengo yake.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2SzD5hM
via

Post a Comment

0 Comments