Ticker

10/recent/ticker-posts

BENKI YA CRDB YAKABIDHI MADAWATI 240 KWA SHULE SITA WILAYANI CHUNYA, MBEYA

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, William Ntimika ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, akipokea sehemu ya madawati kutoka kwa Meneja Mwandamizi wa Benki ya CRDB anayeshughulikia masuala ya Serikali za Mitaa, Suzan Shuma katika hafla iliyofanyika Novemba 30, 2019 katika kitongoji cha LUPA Wilayani Chunya, mkoani Mbeya kwa ajili ya Shule za Sekondari na Msingi zilizomo katika Kata Sita za LUPA, yaliyotolewa na Benki ya CRDB. Jumla ya madawati na Viti 240 vilivyotolewa.
Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, William Ntimika akimkabidhi Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Sophia Kumbuli Madawati yaliyotolewa na Benki ya CRDB kwa ajili ya kata Sita za LUPA Wilayani Chunya katika hafla fupi iliyofanyika Novemba 30, 2019 katika kitongoji cha LUPA Wilayani Chunya, mkoani Mbeya. Kulia ni Meneja Mwandamizi wa Benki ya CRDB anayeshughulikia masuala ya Serikali za Mitaa, Suzan Shuma.
Picha ya pamoja.



from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2Lh6sBk
via

Post a Comment

0 Comments