Ticker

10/recent/ticker-posts

BENKI YA CRDB YA CRDB YAZINDUA MKOPO YA ‘BOOM ADVANCE’ KWA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU

 Benki ya CRDB imezindua mikopo maalum kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo vikuu ijulikanayo kama “Boom Advance”, uzinduzi huo umefanyika katika tamasha la michezo la ‘CRDB Bank – TOT Bonanza’ na kuhudhuriwa na wanafunzi wa vyuo vikuu mbalimbali katika mkoa wa Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi wa Benki ya CRDB, Stephen Adili alisema huduma ya Boom Advance imelenga katika kuwasiaidia wanafunzi kutatua changamoto ya kifedha pindi wawapo vyuoni. “Kwa muda mrefu tumekuwa tukiangalia ni kwa namna gani tunaweza kuipatia suluhisho changamoto hii ambayo kwa kiasi kikubwa imekuwa inachangia kuathiri masomo ya wanafunzi,” alisema Adili.

Adili alisema mkopo huo wa Boom Advance unatolewa kidijitali kupitia huduma yetu ya SimBanking App, ambapo ni njia rahisi itakayowawezesha wanafunzi kufurahia huduma hiyo wakiwa chuoni bila kutembelea benki jambo ambalo lingeweza kuingiliana na muda wa masomo. “Tumefanya hivi tukifahamu kuwa wanafunzi wengi wa vyuo wapo katika kizazi cha kidijitali,” aliongezea Adili.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Stephen Adili akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu ijulikanayo kama 'Boom Advance' uliofanyika wakati wa tamasha la michezo la CRDB TOT Bonanza wikiendi hii.
Ili kupata huduma ya Boom Adavance mwananfunzi anatakiwa kuwa mnufaika wa mkopo kutoka Bodi ya Mikopo HESLB na kusajiliwa katika mfumo wa Benki wa utoaji mikopo kidijitali “Digital Disbursment System”.

Akiongelea baadhi ya sifa na faida za Boom Advance Adili alisema mkopo huo wa Boom Advance unamuwezesha mwanafunzi anaweza kukopa kuanzia TZS 40,000 hadi TZS 120,000 bila riba huku muda wa kurejesha mkopo ukiwa hadi siku 45 tokea kuchukua mkopo, ambapo alisema muda huo umezingatia mpaka mwanafunzi atakapo pata mkopo mwengine kutoka HELSB.
Msheheraji katika uzinduzi wa huduma ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu ijulikanayo kama 'Boom Advance', Meena Ally akipata maoni ya mmoja wa wanufaika wa mkopo huo ambaye ni Mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM, Mbaraka Mohammed uliofanyika wakati wa tamasha la michezo la CRDB TOT Bonanza wikiendi hii. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Stephen Adili na kushoto ni Meneja Mwandamizi wa Bidhaa wa Benki ya CRDB, Edwin Kasali. 
Adili alisema katika mkopo huo wa Boom Advance malipo yanafanyika moja kwa moja baada ya mkopo kuingia kwenye akaunti ya mwananfunzi, lakini pia mwanafunzi anaweza kufanya malipo (yote/sehemu) mwenyewe bila kusubiri hela ya mkopo kutoka HELSB kuingia.

Alizungumza kwaniaba ya wanafunzi wa vyuo vikuu mwanafunzi wa Chuo cha Kodi, Catherine Constatine ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuanzisha huduma hiyo ya Boom Advance huku akisema itakwenda kuwa mkombozi kwa wanafunzi wengi hususan katika kipindi ambacho wanakuwa wakisubiri mkopo kutoka HELLSB au pindi wanapoishiwa fedha.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Stephen Adili (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi na wafanyakazi wa benki hiyo wakati wa uzinduzi wa huduma ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu ijulikanayo kama 'Boom Advance' uliofanyika wakati wa tamasha la michezo la CRDB TOT Bonanza wikiendi hii.
Hivi karibuni Benki ya CRDB pia ilifanya maboresho katika Akaunti ya ya wanafunzi ya scholar ambapo hivi sasa akaunti hiyo haina makato ya aina yoyote, mwanafunzi pia anaunganishwa na mifumo ya kidijitali itakayomuwezesha kupata huduma za benki popote pale alipo ikiwamo TemboCard, SimBanking, Internet banking na CRDB Wakala.

Tamasha hilo pia liliambatana na michezo mbalimbali ambapo timu za mpira wa miguu na kikapu za Benki ya CRDB na timu za vyuo vikuu ziliumana vikali.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/38itaCQ
via

Post a Comment

0 Comments