Ticker

10/recent/ticker-posts

WAZIRI WA AFYA AZINDUA CHUMBA CHA KUHIFADHI MAJOKOFU YA UMEME ZAHANATI YA NYAKASUNGWA SENGEREMA.


***********************************

Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amezindua chumba cha kuhifadhia majokofu yanayotumia umeme wa jua kwenye zahanati ya Nyakasungwa iliyopo halmashauli ya Buchosa wilayani Sengerema.

Halmashauri ya buchosa imepata majokofu 17 kutoka Wizara ya afya mwezi oktoba 2019 kwa awamu ya kwanza na tayari yamesambazwa kwenye na kufungwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Hali ya chanjo kwa halmashauri hiyo kwa kwa mwaka huu ni asilimia 94 kutoka asilimia 79 mwaka jana na katika kampeni ya kitaifa ya chanjo ya surua na rubella mwezi oktoba mwaka huu imefanikiwa kwa asilimia 106.

Majokofu hayo yatasaidia kuimarisha mnyororo baridi na hivuo kuongeza ubora na utunzaji wa chanjo katika vituo vya kutolea huduma za afya ambayo itapelekea watoto kupata chanjo zenye ubora kama ilivyokusudiwa


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2ORt6AY
via

Post a Comment

0 Comments