Ticker

10/recent/ticker-posts

WANAFUNZI WAANAOSOMEA KICHINA WATUNUKIWA TUZO BORA, MAFANIKIO






 Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke akizungumza wakati wa kutoa tuzo kwa wanafunzi ambao wanasoma Lugha ya Kichina pamoja na kozi ya Kichina hapa nchini.Hafla fupi ya kutoa tuzo hizo imefanyika katika ubalozi wa China jijini Dar es Salaam.
Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Wiiliam Ole Nasha akizungumza wakati wa kutoa tuzo kwa wanafunzi wanaosoma Kichina hapa nchini pamoja na kozi za kichina. Tuzo hizo zimetolewa jijini Dar es Salaa katika Ubalozi wa china hapa nchini.
 Mmoja ya wanafunzi walioshindana katika shindano la ubunifu lililofanyika nchini China na kuiuka kidedea katika kuendeleza Teknolojia ya ulishaji wa Samaki, Amos Benjamini akizungumza wakati wa kupewa tuzo kwa wanafunzi wanaosoma Somo la kichina na Kozi ya kichinz
 Mwanafunzi kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam, Gloria Gabriel akizungumza lugha tatu tofauti ili kuwapa uelewa baadhi ya wachina na watanzania waliofika katika hafla fupi ya kuwapa tuzo wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo ya kichina hapa nchuni.
 Baadhi ya washiriki.
 Wageni Waalikwa.
 Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Wiiliam Ole Nasha  akitoa tuzo kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali wanaofanya vizuri katika masomo ya kichina hapa nchini.

 Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke akitoa tunzo kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali hapa nchini kwa kufanya vizuri katika masomo ya kichina, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam katika ubalozi wa China.
 Picha ya Pamoja.
Balozi wa China hapa nchini, Wang Ke akiteta jambo na Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Ole nasha wakati wa utoaji tuzo kwa wanafunzi wanaosoma kichina na kozi za kichina waliopata tuzo bora na tuzo za h

KATIKA kuendeleza ushirikiano wa seikali ya china na Tanzania nchinya china imekuwa miongoni mwa nchi inayotoa ufadhili kwa idadi kubwa ya wanafunzi wa  Tanzania wanaoomba ufadhili wa kusomea kozi mbalimbali nchini china. 

Akizungumza na wakati wa kutoa tuzo ya Balozi , Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke kwa wanafunzi wanaosoma  Lugha ya kichina hapa nchini katika vyuo mbalimbali, amesema kuwa ushirikiano baina ya China na Tanzania unazidi kuimarika zaidi hasa wanafunzi wa Tanzania wanapojifunza Lugha ya Kichina.

"Kwa mwaka huu Serikali ya China limetoa nafasi 302 za ufadhili kwa wanafunzi wanaojifunza kozi mbalimbali nchini". Amesema Wang Ke.

Amesema kuwa Serikali ya China imekuwa nchi inayotoa idadi kubwa zaidi ya nafasi za Ufadhili kwa wanafunzi wa Tanzania.

"Mpaka sasa wanafunzi 1900 wamepata ufadhili wa serikali ya China na kwenda kusoma nchini China miongoni mwao wamehitimu nchini china na wamerudi Tanzania kwaajili ya ujenzi wa sekta mbalimbali hapa nchini". Amesema Wang Ke.

Hata hivyo mmoja wa wanafunzi waliopata ufadhili wa China Amos Benjamini alishiriki katika kambi ya ugunduzi kwa vijana duniani(UNLEASH) yaliyofanyika  Shenzhen aliibuka kidedea kwa kubuni teknolojia ya kulisha Samaki.

Katika tuzo hizo wanafunzi 20 wamepata tunzo bora na wengine 60 wamepata tuzo ya Mafanikio, wanafunzi hao ni kutoka  vyuo mbalimbali.

Hata hivyo Naibu waziri wa Elimu na Teknolojia, Ole Nasha amesema kuwa ushirikiano wa China na Tanzania haujaanza sasa ushirikiano huu ni wa mda mrefu hasa  ukiona Reli ya TAZARA unaweza ukajua ni wa muda gani.

 "Kumekuwa na vijana wengi sana ambao wanasoma kwenye vyuo mbalimbali kwa msaada wa serikali ya nchini china kwahiyo China imekuwa sehemu ya wanafunzi wa kitanzania kwenda kujipatia mafunzo mbalimbali". 

Nasha amebainisha kuwa kwa kwa miaka mitatu  kunawanafunzi zaidi 200 wameenda kusoma kwa msaada wa china.

Nasha amesema kuwa ni fursa kwa wanafunzi wa Tanzania kujua Lugha ya kichina ili waweze kufundisha wanafunzi wengine hapa nchini.

Miongoni mwa waliopata tuzo bora na tuzo za mafanikio wamesema kuwa Lugha ya kichina kwa sasa ipo sokoni kwa mtanzania kujua Lugha mbalkmbali duniani zitamsaidia kupata Ajira hata kwenye makampuni ambayo yanatoa ajira kwa kuzingatia kigezo cha kujua Lugha yao.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2Oeerkz
via

Post a Comment

0 Comments