Ticker

10/recent/ticker-posts

TCRA yahimiza Wananchi kusajili laini za simu kwa alama za vidole mkoani Morogoro

Na Chalila Kibuda,Michuzi Tv.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Mashariki imesema kuwa kila kila mwananchi ajisajili laini yake ya simu  kwa alama za vidole kwani muda uliopangwa unatarajia kuisha hivyo wasiposajili laini zao kwa alama hizo laini itafungwa.

Hayo ameyasema Mwanasheria Mwandamizi wa masuala ya Mawasiliano Vaolet Eseko wakati usajili wa laini za simu kwa alama za vidole  katika Kata ya Mkundi mkoani Morogoro. amesema kuwa kwa sasa wananchi wakamilishe kupata vitambulisho vya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa au kuwa na namba za vitambulisho na kuweza kukidhi matakwa ya kisheria ya kusajili laini kwa alama za vidole.

Mwanasheria huyo amesema kuwa wale ambao walikamilisha awali usajili vitambulisho vya Taifa kufika sehemu yeyote ambako zoezi linaendelea na kwenda kuangalia namba ya utambulisho kwa wale Morogoro na akipata hiyo anasajili laini ya simu kwa alama za vidole.

Amesema kuwa Wananchi ambao hawajapata kufuata taratibu za usajili kwani Ofisi za NIDA kwa kila wilaya za Mkoa Morogoro wanasajili Wananchi.

Aidha amesema kwa  kipindi kilichopo kwa sasa watumie fursa ya kutafuta vitu vya Msingi katika kusajili kwani wasiofanya hivyo laini zao zitafungwa Desemba 31.

Nae wa Mwananchi wa Kata ya Mkundi Angelina Bwakila amesema kuwa kutoa elimu hiyo kumsaidia kupata namba na kuweza kusajili laini za simu.
Amesema Wananchi wafike katika vituo sahihi na kupata taarifa sahihi na sio kuchukua taarifa sehemu zisizohusika.
 Mwanasheria Mwandamizi wa masuala ya Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Mashariki  Vaolet Eseko akizungumza na Wananchi wa Kata ya Mkundi wakati usajili wa laini za simu kwa alama za vidole mkoani Morogoro.
 Wananchi wakiwa katika foleni kuangalia majina yao katika mfumo wa NIDA ili kupata namba na kuwa wamekidhi vigezo vya usajili wa laini za simu kwa alama za vidole.
 Wananchi wakipata huduma ya usajili wa laini za simu kwa alama za vidole katika moja Kampuni ya simu za Mkononi
Mwanasheria Mwandamizi wa masuala ya Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA Vaolet Eseko akitoa maelezo kwa mwananchi kuhusiana na taratibu za kupata kitambulisho Cha Taifa na kuweza kukidhi matakwa ya kisheria ya usajili kwa laini ya simu kwa alama za vidole.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2rZYi9s
via

Post a Comment

0 Comments