Ticker

10/recent/ticker-posts

TAWI LA YANGA MAFINGA WAKABIDHI TANKI NA PAMPU ZA MAJI KWA SHULE YA SEKONDARI IYONGOLE

Mbunge wa Mafinga Cosato Chumi amewapongeza Wanachama wa Yanga Tawi la Mafinga, maarufu kama Vanyalutogo kwa juhudi za kutatua changamoto katika jamii.

Chumi amesema kitendo walichokifanya ni uwanamichezo uliotukuka  ambapo kwanza walianza na tanki la.maji na sasa wameleta pampu za kuvutia maji.

“Hongereni sana Yanga Mafinga, huu ni uwanamichezo uliotukuka, kwanza mlianza na Tanki la maji, lakini tena mkajiongeza mumekabidhi na pump.  Huu ni uzalendo wa kimichezo.”amesema Chumi.

 Tawi hilo la Mafinga limetoa msaada wa Tanki la Maji na Mashine ya kuvuta maji (Water Pump) kwa Shule ya Sekondari ya Iyongole.

Wanachama hao wakiongozwa na Mwenyekiti wao tawi Gift Mwachang'a wamwtoa vifaa hivyo kwa wanafunzi ili kiutatua changamoto ya maji kwenye shule hiyo.

 “Vifaa hivi vyote vimetolewa na Wanayanga wenyewe, hii ni Timu ya Wananchi na tunawafikia Wananchi kwa namna mbalimbali,” Mwachang’a.
 



from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2KWCEtB
via

Post a Comment

0 Comments