Ticker

10/recent/ticker-posts

Shabiki Yanga, Barcelona ashinda Milioni 76.2 za M-BET

Dar es Salaam.Shabiki wa timu ya kongwe ya soka nchini, Yanga, Barcelona na Manchester City, Samson Auzebio Mlembe (23) ameshinda Sh 76, 200, 750 kupitia mchezo wa Perfect 12 wa kampuni ya M-BET.

Msemaji wa kampuni ya M-Bet Tanzania David Malley amesema kuwa Mlembe ameshinda fedha hizo baada yakubashiri kwa usahihi mechi 12 za ligi mbalimbali duniani.

Malley alisema kuwa Mlembe ambaye ni mkazi wa Dodoma amekuwa mshindi wa tano kwa mwezi Novemba na 17 miezi 11 na kuweza kubadili maisha yao kupitia mchezo wa Perfect 1.

Alisema kuwa M-BET ni inaendelea kuwa nyumba ya mabingwa kwa kutoa washindi wengi zaidi ambapo mpaka sasa wametumia zaidi ya Sh milioni 700 kwa washindi na bonusi kwa mwezi Novemba peke yake.

“Tunazidi kuinua vipato kwa Watanzania, tumeweza kutoa zaidi ya mamilioni ya fedha kwa mwezi huu na kuwa kampuni pekee iliyoweza kutoa fedha nyingi kwa washindi,” alisema Malley.

Kwa upande wake, Mlembe alisema kuwa hakufikiria kabisa kuwa Allen Mushi kuwa ni tapeli wa mjini baada ya kupokea simu yake.Mlembe alisema kuwa anamfahamu Mushi kutokana na kumuona akiwakabidhi fedha washindi wengi Perfect 12 na kuamini kuwa ameshinda.

“Mpaka sasa sijapanga nitumie fedha hizi kwa mambo gani, ni fedha nyingi ambayo sikutegemea kuipata, nitakaa na wazazi wangu na kujua nini cha kufanya, kwa kweli siwezi kukurupuka,” alisema Mlembe.

Alisema kuwa kuna biashara mbalimbali za kufanya, lakini lazima uweke mikakati na mipango sahihi kabla ya kuanza.
Msemaji wa Kampuni ya M-BET Tanzania, David Malley (kulia) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Sh milioni 76.2 Mkazi wa Dodoma, Samson Mlembe aliyeshinda mchezo wa kubashiri wa Perfect 12. Katikati ni Shabani Mwanga, Mkuu wa Kitengo cha Kodi za Michezo ya Kubahatisha (TRA), mkoa wa kodi wa Ilala.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2XWBseM
via

Post a Comment

0 Comments