Ticker

10/recent/ticker-posts

NANDY APISHANA NA RAIS DKT MAGUFULI

Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Faustina Mfinanga Maarufu kama Nandy anayetamba na wimbo wake mpya wa Magufuli amepishana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Nandy aliyetakiwa kutumbuiza leo katika ufunguzi wa Mkutano wa mawaziri wa Mambo ya Nje 34 wa nchi za Afrika 29 na nchi tano za Nordic ameshindwa kufanya hivyo baada ya kuchelewa kufika na kutokuruhusiwa kuingia ndani.

Taarifa zinasema, Nandy alitakuwa kuwasili mapema saa 2 asubuhi kabla Rais hajafika ila alijikuta anafika saa 3 na tayari ufunguzi wa Mkutano huo ukiwa umeanza.

Kutokana na tukio hilo, nenda ambaye alikua ni msanii.pekee aliyetakiwa kutumbuiza kwenye ufunguzi huo ameshindwa baada ya kushindwa kufika kwa muda aliopangiwa.

Nandy amekuwa ni miongoni mwa wasanii waliopata fursa ya kutumbuiza katika mikutano mikumbwa mbalimbali na kibao chake kipya kiitwacho Magufuli

Rais Dkt Magufuli amefungua mkutano wa mawaziri wa Mambo ya Nje 34 wa nchi za Afrika 29 na nchi tano za Nordic ambao umeanza Novemba 8 mwaka huu nchini Tanzania.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2qusQ2t
via

Post a Comment

0 Comments