Ticker

10/recent/ticker-posts

Nakwenda kufanya Kilimo ,Watu wa mjini wakinihitaji nitakuja- CAG Mstaafu Profesa Assad

CAG mpya Kichere- kazi yangu ni kulinda kihenge cha mapato ya serikali


Na Chalila Kibuda, Michuzi TV

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) aliyemaliza muda wake Profesa Mussa Assad amesema kuwa anakwenda kufanya kilimo kutokana na uwekezaji alioufanya katika siku hivi karibuni baada ya kustaafu nafasi hiyo watu mjini wakinihitaji nitakuja .

Profesa Assad ameyasema hayo wakati wa makabidhiano na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mpya Charles Kichere katika hafla iliyofanyika kwenye Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT),leo  jijini Dar es Salaam.

Profesa amesema kuwa katika kufanya kazi amewashukuru wafanyakazi wa ofisi hiyo kwa ushirikiano waliompa katika kipindi chote cha utumishi na kumtaka CAG mpya afanye ushirikiano nao kwani watu hao wamejengwa kwa muda mrefu na sifa zote .

Assad amesema kuwa katika kufanya kazi tumejenga mahusiano na wadau mbalimbali wa nje ambao ndio watu wa kujengeana uwezo na sio kwa ndani

“Changamoto ni nyingi tumepitia lakini siwezi kutia ukakasi katika hili na watu  niliowakosea, naomba wanisamehe kwani sisi ni binadamu”amesema Profesa Assad

Kwa upande wa CAG Charles Kichere mpya amesema kuwa kazi kubwa ni kulinda kihenge anajua kazi ngumu ya ukusanyaji wa mapato.

Kichere amesema ataifanya kazi hiyo kwa weledi na uadilifu kwa kushirikiana na timu yake ya ofisi ya Taifa ya mkaguzi ikiwa na kuangalia mapato ya nchi yanatumikaje kwa kuangalia ripoti sambamba na kujenga timu imara na sio watu walisambaratika.
Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali aliyemaliza muda wake Profesa Mussa Assad akimkabidhi nyaraka za ofisi CAG mpya Charles Kichere katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam. 
Mkaguzi na Mdbiti Mkuu wa Hesabu za Serikali aliyemaliza muda wake Profesa Mussa Assad akizungumza mara baada ya makabidhiano ya nyaraka na CAG mpya Charles Kichere katika hafla iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) mpya Charles Kichere akizungumza mara baada ya kukabidhiwa na aliyekuwa CAG Profesa Mussa Assad katika hafla iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) Mpya Charles Kichere akiwa na maua mara baada ya kupokewa wakati akiwasili katika ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kwa ajili ya makabidhiano ya Ofisi ya aliyekuwa CAG Profesa Assad jijini Dar es Salaam.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2WNAml1
via

Post a Comment

0 Comments