Ticker

10/recent/ticker-posts

MRADI WA MIAKA MITANO UZALISHAJI BORA WA MAZIWA KUONGEZA SOKO LA BIDHAA WAZINDULIWA NCHINI

TANZANIA kwa kushirikiana na taasisi ya kimataifa ya uwezeshaji mifugo ya maziwa ya Land o'lakes imezindua mradi wa miaka mitano wa uzalishaji bora maziwa na kuongeza soko la bidhaa za maziwa nchini ifikapo mwaka 2025. 

Akizundua mradi huo jijini dar es salaam Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Elisante Ole Gabriel amesema mradi huo unazingatia uwezeshasji kwa maafisa ugani mikoa 26 ya Tanzania bara na kwamba utaanza kutekelezwa katika mikoa minne ya Dar es salaam, Pwani, Tanga na Morogoro. Prof. Elisante Ole Gabriel amesema mradi huo utazingatia kuwezesha maafisa ugani, pembejeo na uzalishaji wenye tija hadi kufikia mahitaji ya soko la bidhaa za maziwa ndani na nje ya nchi.

Prof. Elisante Ole Gabriel amesema mradi huu ambao unaungwa mkono na ichi kadfha za wahjidsani ikiwemo marekani unalenga [pia luunga mkono juhudi za rais wa awamu ya tano mhe. Dk John Pombe Magufuli katika kuhakikisha nchi inakuwa katika uchumi wa viwanda na kujitegemea kiuchumi. Amesema kwa sasa Tanzania bado ina uzalishaji mdogo wa maziwa licha ya kuwa na idadi kubwa ya mifugo huku wafugaji na sekta ya kilimo ikiabiliwa na changamoto za ugani anautaja mradi huu kuja na ufumbuzi wa wa kuhakikisha uzalishaji maziwa unaongezeka mara dufu.

Hata hivyo prof. OLE GABRIEL anawataka watanzania kupokea mradi huu kwa mikono miliwi na kuondokana na ufugaji wa k,uchunga kuelekea ufugaji wa kibiashara na kuiwesha nchi kungezea thamani bidhaa za maziwa kwa mahitaji ya ndani na nje ya nchi

Kwa idha prof GABRIEL amesema kwa mujibu wa takwimu za mwaka huu Tanzania inao mifugo ngombe milioni 30 mbuzi milioni 20.5 kondoo million 5.5 lakini wanaotumika katika uzalishaji maziwa ni milioni mbili tuu

Kwa upande wa mratibu wa mradi huo nchini Tanzania kutoka taasis ya LAND O’LAKES bi. Neema mrema amesema mradio pia unatekelezwa katika nchi kadhaa baranmi afrika ambapo umeonyesha mafanikio makubwa kwa kuinua pato la wafugaji na nchi husika kwa ujumla.

Amesema taasisi hiyo ya kimataifa imekuwa ikitekeleza miradi hiyo kwa kuwaeeshesha maafisa ugani na pembejeo za kisasa kwa manufaa ya kuleta tija kwa ongezeko la maziwa kutoka ng”ombe mmoja kukamuliwa lita 5 hadi 15 kwa siku


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2OuT9Oo
via

Post a Comment

0 Comments