Ticker

10/recent/ticker-posts

MKUTANO WA WAFADHILI WA TAFITI KUFANYIKA MEI, 2020, NCHINI AFRIKA KUSINI, MKUTANO WA DAR WAFUNGWA

 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolijia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati wa ufunga mkutano wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu uliokuwa ukifanyika kuanzia Novemba 11-15 katika Hoteli ya Serena. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya utafiti ya taifa nchini Afrika Kusini, Dkt. Molapo Qhobela.

Na Avila Kakingo, Globu ya jamii.
MKUTANO wa sayansi, teknolojia na ubunifu wa fungwa jijini Dar es Salaam ikiwa ni mwendelezo wa Mkutano wa mkubwa utakaofanyika nchini Afrika ya Kusini Mei 2020 kwa nchi zote duniani zinazofadhili utafiti katika nchi mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolijia (COSTECH), Dkt. Amos Nungu, amesema kuwa sasa wako kwenye maandalizi ya mkutano wa kimataifa wa nchi zinazofadhili utafiti dunianikote.

"Leo tulikutunajadili kuhusiana na maandalizi ya mkutano mkuu utakaofanyika Afrika Kusini hapo 2020" utakaohusisha mataifa yanayofadhili utafiti duniani kote".

Pia Dkt. Nungu amewaasa wanaofanya utafiti wa kisayasni waaswa kufanya tafiti zinazotatua matatizo ya jamii na sio matatizo ya leo tuu.

Amesema kuwa katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam wamejadili mambo mbalimbali ili kuboresha tafiti kwa kila nchi ya kusini mwa Jangwa la Sahara.

"Tulikuwa tunaangalia mifumo ya maendeleo na ubunifu, uwekezaji kwenye utafiti kwaajili ya maendeleo ya nchi zetu tumejadili kwa mapana kubadilishana uzoefu, lakini Pia tuliangalia kwa hawa wafadhili kuwa na mashirikiano yenye usawa wakati wa kufanya utafiti".

Hata hivyo Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya utafiti ya taifa nchini Afrika Kusini, Dkt. Molapo Qhobela amesema kuwa Mkutano huu umefanikiwa sana nchi 15 za kusini mwa jangwa la Sahara za utafiti kwa Dar es Salaam tumefanikiwa kujadili mada mbalimbali na kubadilishana uzoefu wa kitafiti.

Dkt Molapo Amesema kuwa kwa Tanzania Tumemaliza kwa mafanikio makubwa na kwa mwakani 2020 utafanyika nchini Afrika Kusini.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/330doIN
via

Post a Comment

0 Comments