Ticker

10/recent/ticker-posts

MBUNGE AYSHAROSE MATTEMBE AONGOZA CHANGIZO UJENZI WA MADARASA NA UFUNGUZI WA SHULE ITIGI



Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe (katikati), akikata utepe kuashiria kufungua rasmi Shule ya Msingi Mitundu 'B' iliyopo wilayani Itigi mkoani humo baada ya kupata usajili wa Serikali ambapo pia aliendesha harambee ya kupata fedha za ujenzi wa madarasa mawili ya shule hiyo. Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Ally Minja, Mwalimu Mawazo Myabhi, Afisa Mtendaji wa Kata ya Mitundu, Raphael Ackley na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Manyoni, Blandina Mawala. 
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akisalimiana na Mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, Timothy Yona.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akiwasalimia wananchi kwa kuwapungia mikono.

Wanafunzi wakipiga makofi wakati wa kumpokea mgeni rasmi Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe 
Wimbo wa Taifa ukiimbwa.
Wanafunzi wakiimba wimbo maalumu.
Wazazi na walezi wakiwa kwenye hafla hiyo.
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, William John akizungumza.
Wanafunzi wakifurahi kwenye hafla hiyo.
Mratibu Elimu wa Kata hiyo, Sister Christina Muro, akizungumza.
Chifu wa Kata hiyo, Mzee Ally Idd Izenzele, akizungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Manyoni, Abel Mtaalamu, akizungumza.
Sister Salome Timothy Nkowi, akimkabidhi zawadi Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe.
Wanawake wa UWT wakimkabidhi zawadi ya kitambaa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Ally Minja, akikabidhiwa zawadi.

Twist ikichezwa.
Mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo, Timothy Yona, akizungumza.
Katibu wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Manyoni, Mwadawa Maulid, akizungumza.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Manyoni, Blandina Mawala, akizungumza.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Ally Minja, akizungumza.
Watoto nao walikuwepo kwenye hafla hiyo.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe (katikati), akiongoza harambee hiyo. 
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akisisitiza jambo kwenye changizo hilo.
Mshereheshaji wa hafla hiyo (MC) Mwalimu Utukufu Gwimile akiwajibika
Diwani wa Viti Maalumu (CCM) wa kata hiyo, Rose Madumba, akizungumza.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mitundu, Benjamin Lissu, akizungumza kwa niaba ya walimu wenzake wakati wakichangia harambee hiyo.
Saruji ikiletwa kwenye harambee hiyo.


Mdau wa maendeleo wa kata hiyo, Mhandisi Felix Dagaki, akizungumza kwenye harambee hiyo.







Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akimkabidhi mpira Mwalimu Paul Maduhu kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo.



Hafla ikiendelea.



Muonekano wa majengo ya shule hiyo.








Na Dotto Mwaibale, Singida





JAMII imetakiwa kuwekeza kwenye miundombinu ya shule ili wanafunzi waweze kupata elimu katika mazingira bora.





Ombi hilo limetolewa jana na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe wakati akiendesha harambee ya kupata fedha za ujenzi wa madarasa mawili ya Shule ya Msingi Mitundu 'B' iliyopo wilayani Itigi mkoani humo wakati akiifungua rasmi baada ya kupata usajili wa Serikali.





"Nawaombeni wazazi na walezi wekezeni katika kuboresha miundombinu ya shule ili watoto wapate elimu katika mazingira bora" alisema Mattembe.





Mattembe alisema urithi pekee wa kumpa mtoto ni elimu na sio nyumba wala pesa hivyo kila mwanajamii anapaswa kuguswa katika kuchangia ujenzi wa miundombinu ya shule.





Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Ally Minja alisema bila ya kufanya jitihada za makusudi za ujenzi wa madarasa katika Kata hiyo ya Mitundu hali itakuwa mbaya kutokana na ongezeko kubwa la watoto ambapo kwa mwezi watoto kati ya 80 hadi 95 wanazaliwa.





"Hapa Mitundu pana uchumi mkubwa hivyo tusipo jitoa katika ujenzi wa vyumba vya madarasa tutashindwa pa kuwapeleka watoto wetu kupata elimu au watalazimika kurundikana katika darasa moja watoto zaidi ya 200" alisema Minja.





Minja alisema idadi ya watoto wanaozaliwa katika kata hiyo ni kubwa ukilinganisha na ongezeko la vyumba vya madarasa na idadi hiyo ni kwa watoto waliosajiliwa baada ya mama zao kujifungua katika kituo cha afya cha kata hiyo.





Mdau wa maendeleo wa kata hiyo, Mhandisi Felix Dagaki ambaye alitoa sh.milioni moja na saruji mifuko 20 kuchangia ujenzi wa madarasa hayo aliwataka wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii na kuwa wao ndio wanategemewa kuwa viongozi wa kesho kwani hata yeye alisoma katika kata hiyo.





Katika harambee hiyo Mattembe alichangia sh.500,000 na fedha taslimu zikiwa ni sh. 215,000 , ahadi ikiwa ni sh. Milioni 2, 215,000 na saruji mifuko 24.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2PGBHst
via

Post a Comment

0 Comments