Ticker

10/recent/ticker-posts

MBUNGE AYSHAROSE MATTEMBE AKAGUA KITUO CHA AFYA NA UJENZI WA SHULE ITIGI SINGIDA

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe akishiriki ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi Isingiwe wakati alipofanya ziara ya kukagua Kituo cha Afya cha Kata ya Mitundu na ujenzi wa vyoo vya Shule ya Sekondari ya Mitundu iliyopo wilayani Itigi mkoani Singida juzi. 
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akikagua ujenzi wa vyoo vya Shule ya Sekondari ya Mitundu.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akikagua Hosteli wanayoitumia wanafunzi wa kike wa Shule ya Sekondari ya Mitundu.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akizungumza na wanafunzi wa kike ambao wapo hosteli na kuwasisitizia kuzingatia masomo.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akisalimiana na Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Mitundu, Sister Sarah Tidias alipofika kukagua kituo hicho. Kusho ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Ally Minja.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akiingia kukagua chumba cha kuhifadhia dawa cha kituo hicho.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akikabidhi mashuka katika kituo hicho.
Mashuka yakikabidhiwa.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Aysharose Mattembe, akikabidhi sabuni.
Madarasa mawili yaliyo kwisha kujengwa Shule ya Msingi Isingiwe. 


Na Dotto Mwaibale, Singida

MBUNGE wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida Aysharose Mattembe amekagua Kituo cha Afya cha Kata ya Mitundu na ujenzi wa Shule ya Msingi Isingiwe na ujenzi wa vyoo Shule ya 

Sekondari ya Mitundu iliyopo wilayani Itigi mkoani Singida na kuzungumza na mganga mfawidhi wa kituo hicho Sister Sarah Tidias ili kujua changamoto zilizopo.

Akizungumzia changamoto zilizopo katika kituo hicho Sister Tidias alisema wanaukosefu wa maji ambapo hutumia kutoka kwenye visima viwili ambayo huyavuta kwa kutumia mikono na 

kuwa hakina umeme mbadala baada ya wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kukatika."Umeme wa Tanesco ukikatika tunalazimika kutumia tochi kumsaidia mjamzito wakati wa kujifungua" alisema Sister Tidias.

Tidias alitaja changamoto nyingine kuwa kituo hicho kina watumishi wachache, hakina gari la kubebea wagonjwa kwa ajili ya kuwapeleka Hospitali ya Rufaa.

Alitaja changamoto nyingine kuwa wanauhaba wa majengo kama jengo la upasuaji, wodi ya watoto, wodi ya wanawake na wanaume, jengo la kufulia, kuhifadhia maiti, nyumba za watumishi na uzio kuzunguka kituo hicho.

Alitaja huduma zinazotolewa katika kituo hicho kuwa ni kutibu wagonjwa wa nje ambao kwa mwezi ni hufikia 800 na zaidi, wajawazito ambao kwa mwezi uliopita walikuwa 95 na kliniki ya watoto kwa mwezi wanahudumia watoto 120.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/34sPSFF
via

Post a Comment

0 Comments