Ticker

10/recent/ticker-posts

DOKTA KIJAJI AKITAKA CHUO CHA MIPANGO KUFANYA UTAFITI WA UMASIKINI NA UTEKELEZAJI MIRADI YA UMMA

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza na Wahitimu na watumishi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, katika mahafali ya 33 ya Chuo hicho ambapo aliuagiza uongozi wa chuo hicho kuongeza juhudi katika masuala ya tafiti zinazolenga kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo na kupunguza umaskini.
Kamishina Msaidizi wa Bajeti kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Pius Mponzi, akitoa neno la kumkaribisha mgeni rasmi wa mahafali ya 33 Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani), kwa niaba ya Katibu Mkuu waWizara hiyo.
Mkuu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini, Prof. Hozen Mayaya akitoa hotuba katika Mahafali ya 33 Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma.
Baadhi ya Wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya 33 ya chuo hicho.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akimtunuku Shahada ya Mipango na Usimamizi wa Mazingira mmoja wa wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, katika Mahafali ya 33 ya chuo hicho ambapo aliwasihi wahitimu hao kutumia elimu waliyoipata kujiajiri.
Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma wakivaa kofia baada ya kutunukiwa Astashahada na Shahada mbalimbali katika Mahafali ya 33 ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere chuoni hapo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akipokea zawadi ya mipira kutoka kwa Mkuu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini, Prof. Hozen Mayaya katika Mahafali ya 33 ya Chuo hicho Kampasi Kuu ya Dodoma, mipira hiyo imetengenezwa katika kiwanda cha kujenga kiwanda cha kuchakata na kutengeneza bidhaa za ngozi katika kijiji cha Idifu Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma ambapo Chuo kimewekeza jumla ya shilingi milioni 396.
Mfanyakazi wa Wizara ya Fedha na Mipango Mike Luzigah (katikati) akiwa na baadhi ya Wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu wafuatilia kwa karibu matukio mbalimbali ya kutunukiwa Astashahada na Shahada mbalimbali katika Mahafali ya 33 ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere chuoni hapo.

Jumuiya ya Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, wakimsikiliza Mkuu wa Chuo hicho Prof. Hozen Mayaya, akitoa hotuba wakati wa Mahafali ya 33 ya Chuo hicho ambapo wahitimu 3,182 wa,etunukiwa Astashahada na shahada mbalimbali.



(Picha na Farida Ramadhani-Wizara ya Fedha na Mipango)

…………………..

Benny Mwaipaja, Dodoma

NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, amekitaka Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, kutafiti kwa kina namna wananchi wanavyoweza kuondokana na umasikini wa kipato pamoja namna Miradi mbalimbali ya Serikali inavyoweza kutekelezwa kwa ufanisi na kwa kuzingatia thamani ya fedha kuliko ilivyo sasa.

Dkt. Kijaji ametoa rai hiyo wakati akiwatunuku astashahada na shahada mbalimbali wahitimu 3,182 Wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Kampasi ya Dodoma wakati wa sherehe za mahafali ya 33 ya chuo hicho.

Amesema kuwa matokeo ya tafiti hizo yataisaidia Serikali na Jamii kwa ujumla kupanga mikakati ya namna ya kukabiliana na umasikini wa wananchi hususan wa vijijini pamoja na kuharakisha maendeleo ya nchi kwa kuhakikisha kuwa miradi inayotekelezwa na Serikali inakuwa na tija.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango ambaye pia ni Kamishna Msaidizi wa Bajeti Bw. Pius Mponzi amemwahidi Dkt. Ashatu Kijaji, kwaniaba ya Baraza la Chuo hicho kwamba wataongeza jitihada katika eneo la utafiti na kuhakikisha kuwa matokeo ya utafiti huo yanawafikia wananchi kwa lugha rahisi

Naye Mkuu wa Chuo hicho cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Profesa Hozen Mayaya amesema chuo chake kimetimiza miaka 40 tangu kianzishwe na kimepata mafanikio makubwa kwa kutoa wahitimu mahili na wenye kukidhi mahitaji ya soko.

Amebainisha kuwa Chuo kimeongeza idadi ya kozi kutoka kozi moja mwaka 1980 hadi kufikia kozi 25 mwaka huu, huku idadi ya wanachuo wanaodahiliwa nayo imeongezeka kutoka wanachuo 13 mwaka huo hadi kufikia wanachuo zaidi ya elfu 11 mwaka huu.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2Dxd1ve
via

Post a Comment

0 Comments