Ticker

10/recent/ticker-posts

CHOMBO CHA MAJI CHA FADHILI MIRADI 119, BARA LA AFRIKA

Waziri wa maji na umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa mawaziri wa maji wa bara la Afrika jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya mawaziri wa bara la Afrika wakimsikiliza moja ya watoa maada katika mkutano wa mawaziri wa bara la Afrika wanaoshughulikia maji.

MAWAZIRI wa maji wa bara la Afrika wakutana jijini Dar es Salaam kujadili mpango ya maendeleo ya maji safi na maji taka katika nchi za bara la Afrika.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mawaziri wa wa maji wa bara la Afrika jijini Dar es Salaam leo, Waziri wa maji na umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa amesema kuwa Chombo cha Maji cha Afrika kianzishwa kwa lengo la kuchangia maendeleo ya maji na usafi wa mazingila kwa nchi za Afrika.

Mbarawa amesema kuwa chombo hicho kilianzishwa 2006 hadi leo na kimemeshafadhili miradi 119 katika bara la Afrika na imegharimu zaidi ya uro milioni 156.

"Chombo cha Maji kwa upande wa Tanzania kimesaidia kuchimba bwawa lililosimamiwa na Tanesco, bwawa la kikongwe na takribani uro milioni moja nukta tisa sita (1.96) pia chombo hiki ndicho kilicho simamia mradi wa maji safi na salama cha Arusha uliogharimu shilingi bilion 520, ambapo mradi huo utakapomalizika utasaidia na kubadilisha maisha ya wakazi wa Arusha hasa kwenye eneo la maji safi na salama pia maji taka".Amesema Profesa Mbarawa

Profesa Mbarawa amesema kuwa kupitia chombo hicho wataweza kutoa fedha kwaajili upembuzi yakinifu kwenye mabwawa yanayotarajiwa kujengwa Songwe kwaajili ya kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi wa Tanzania na Malawi.

Hata hivyo Profesa Mbalawa amesema kunajuhudi mbalimbali katika chombo hicho za kutafuta fedha kwaajili ya kuunganisha nchi zote kwa juhudi ya pamoja kwaajili ya kutafuta maji kwa nchi zote za Afrika ili huduma ya maji iwafikie watu wote.

Changamoto kubwa inayowakumba chombo hicho cha maji cha bara la Afrika ni kuwashirikisha sekta binafsi  katika huduma ya maji safi na salama pamoja na uongeza ubunifu katika miundombinu ya huduma ya maji na usafi wa mazingira.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2sggYC7
via

Post a Comment

0 Comments