Ticker

10/recent/ticker-posts

CCM Tabora Yajitamba Katika Uchaguzi Wa Serikali Za mitaa



Na, Editha Edward -Tabora

Wagombea wote wa chama cha mapinduzi katika uchaguzi wa Serikali za mitaa mkoani Tabora wamepita kwa asilimia 95 bila ya kukosa wapinzani kutokana na vyama vingine kutoweka na Wagombea wengine kujitoa 

Hayo yamebainishwa na katibu wa CCM Mkoa wa Tabora Solomoni Kasaba alipokuwa akizungumza na blog hii ofsini kwake

Amesema kuwa hata kabla ya kuingia kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji mkoani hapo asilimia 95 ya Wagombea wote wa CCM wameshapita bila kupingwa asilimia 5 tu ndio watakaofanyiwa uchaguzi 

Katika hatua nyingine amefafanua kuwa kati ya vijiji 715 vya Mkoa mzima CCM imekosa wapinzani katika vijiji 675 hivyo Wagombea wake watapita bila kupingwa, huo ukiwa Ni ushindi wa asilimia 94.7 na uchaguzi utafanyika katika vijiji 38 tu sawa na asilimia 5.3

Aidha amebainisha kuwa kati ya mitaa 148 ya Mkoa mzima Wagombea 140 wa CCM wamepita bila kupingwa huo ukiwa Ni ushindi wa asilimia 94.5 hivyo uchaguzi utafanyika katika mitaa 8 tu ambayo Ni sawa na asilimia 5.5

Katika upande wa Vitongoji Solomoni Amesema kati ya vitongoji 3619 vya Mkoa mzima Ni vitongoji 3397 wamepita bila kupingwa hivyo uchaguzi utafanyika katika vitongoji 228 tu sawa na asilimia 6

Aidha  ametaja vyama vitakavyochuana na CCM kuwania nafasi hizo kwa baadhi ya maeneo kuwa ni NRA,  CCK, CHADEMA, CUF, Democratic Part, Demokrasia Makini, NCCR Mageuzi  na ADA TADEA. 
Katibu wa CCM Mkoa wa Tabora Solomoni Kasaba.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/34jjk12
via

Post a Comment

0 Comments