Ticker

10/recent/ticker-posts

BRELA YASHIRIKI MKUTANO WA KIKANDA WA WATALAAMU WA MASUALA YA MILIKI BUNIFU AFRIKA KUSINI

KAIMU Mkuu wa Kitengo cha Leseni za Biashara- (wanne kutoka kushoto) Tawi Kilumile ndiye Mwenyekiti wa Mkutano huo unaohusisha nchi 15 wanachama wa SADC Mkutano huo Tanzania imewakilishwa na Bakari Mketo Mkurugenzi wa Huduma na Uwezeshaji wa BRELA (wa kwanza kulia mstari wa pili)

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) iliyopo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara imeshiriki kwenye Mkutano wa wa Kikanda Wataalamu wa masuala ya Miliki Bunifu kwa nchi za jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Africa (SADC) Johannesburg- Afrika Kusini tarehe 25-26 Novemba, 2019.

Lengo la Mkutano huo ni Kuandaa Mpango kazi wa Utekelezaji wa Mkakati (Framework) na Taratibu za kusimamia na kutumia Miliki Bunifu katika Utekelezaji wa Mkakati wa Viwanda wa nchi wanachama wa Jumuiya ya SADC.

Tanzania kwa Heshima iliyowekwa na Rais ambaye ndiye Mwenyekiti wa SADC Bw. Mh Dr. John Pombe Joseph Magufuli Tanzania imepewa heshima ya kuwa Mwenyekiti pia wa Mkutano huo

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni -BRELA imewakilisha nchi katika Mkutano huo kwa kuwa ndiyo Ofisi ya Taifa ya Miliki Bunifu (National IP Office)


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/34jr57q
via

Post a Comment

0 Comments