Ticker

10/recent/ticker-posts

BREAKING NEWZZZZZ: MAHAKAMA YAAMURU WABUNGE WANNE WA CHADEMA WAKAMATWE


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru wabunge wanne wa Chadema wakamatwe na kufikishwa mahakamani hapo kwa kukiuka masharti ya dhamana.

Wabunge hao ambao ni washtakiwa katika kesi ya uchochezi namba 112ya mwaka 2018 ni Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini, John Heche mbunge wa Tarime Vijijini, Christopher Msigwa Mbunge wa Iringa Mjini na Halima Mdee Mbunge wa Kawe.

Amri hiyo imetolewa leo Novemba 15, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba kufuatia washtakiwa hao kutofika Mahakamani hapo wakati kesi yao ilipokuja kwa ajili ya kusikilizwa bila ha kuwepo taarifa zozote kutoka kwao wala wadhamini wao.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2rHmr4w
via

Post a Comment

0 Comments