Ticker

10/recent/ticker-posts

Bei ya korosho yaongezeka

Bei ya korosho kwa mnada wa pili  umeongezeka na kufikia 2717 kwa kilo moja ambapo mzigo wote uliopo tan 13,115  umeuzwa

Akitangaza Bei hiyo Meneja Mkuu wa TANECU Mohamed Mwinguku amesema kuwa korosho zilizopo kwenye maghala ya Chama Cha Ushirika Tandahimba na Newala (TANECU) zimenunuliwa zote

Amesema kuwa korosho kwa Wilaya ya Tandahimba imenunuliwa kwa sh 2717 kwa mnunuzi wa kwanza,wapili kanunua kwa sh 2697 na mnunuzi wa tatu amenunua kwa sh 2658  

"Korosho iliyopo maghalani tayari tumeiuza yote kwa makampuni matatu Kati ya makampuni 37 yaliyojitokeza," amesema Mwanguku

Naye mkulima Hamis Hassan amesema pamoja na ongezeko Hilo malipo yafanyike kwa muda muafaka ili fedha zimfikie mkulima kwa wakati.

Katika mnada huo makampuni 37  na yalijitokeza,mnada mwingine wa tatu unatarajiwa kufanyika Wilaya ya Newala.

 Meneja wa Chama Cha Ushirika Tandahimba na Newala (TANECU) Mohamed mwinguku akizungumza na w
Wadau wa zao la korosho wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/32sXVRy
via

Post a Comment

0 Comments