Ticker

10/recent/ticker-posts

WAZIRI MHAGAMA AKAGUA MAANDALIZI YA KILELE CHA MBIO ZA MWENGE WA UHURU – LINDI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akieleza jambo kwa Wanakamati ya Maandalizi alipotembelea Uwanja wa Ilulu kukagua maandalizi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru zinazotarajiwa kufanyika Mkuani Lindi. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alipotembelea uwanja wa Ilulu kukagua maandalizi ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru. Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Andrew Massawe.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na watoto wa halaiki alipowatembea kwa ajili ya kukagua maandalizi yao kuelekea Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Sehemu ya watoto wa halaiki wakifanya mazoezi ya utayarisho kuelekea Kilele cha mbio za mwenge wa Uhuru zinazotarajiwa kufanyika Mkoani Lindi Oktoba 14, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akipokea mwamvuli kutoka kwa Meneja wa Kampuni ya Simu ya Airtel Tanzania kanda ya Lindi Bw. Zephania Ludigija itakayotumiwa na Watoto wa Halaiki.PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/35m4eJ2
via

Post a Comment

0 Comments