Ticker

10/recent/ticker-posts

WAZIRI JENISTA: WAAJIRI ZINGATIENI USALAMA WA WAFANYAKAZI WENU MAHALA PA KAZI KUEPUSHA AJALI NA MAGONJWA

Mkaguzi wa Afya ya Mazingira kutoka OSHA, Glory Boniventure akimuelezea Mhe. Jenista Mhagama Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, matumizi ya Vifaa ambavyo vimetolewa na Shirika la Kimataifa la Workplace, Health Without, Borders (WHWB) vitakavyotumiwa na Wakaguzi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, akiwa na kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Khadija Mwenda kwenye Kufunga Mafunzo Kwa Wakaguzi wa OSHA Jijini Arusha.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi,Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama, amewataka wamiliki wa maeneo ya kazi kuzingatia usalama na Afya mahali pa kazi kwa Wafanyakazi wao.

Akizungumza katika hafla ya kufunga Mafunzo maalumu ya Usalama na Afya mahali pa Kazi kwa wakaguzi wa OSHA yaliyofanyika jijini Arusha, Mhe. Mhagama amesema kila ajira zinapozalishwa zinaenda sambamba na ajali pamoja na magonjwa, amesema hivyo waajiri wanapaswa kuhakikisha wanazingatia usalama wa wafanyakazi wao, amesema kukua kwa haraka kwa teknolojia inayotumika viwanda na maeneo mengine ya kazi kunagusa moja kwa moja afya na usalama wa wafanyakazi.

Naye Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi Khadija Mwenda amesema, walishirikiana na Shirika la Kimataifa la Workplace Health Without Borders (WHWB) katika mafunzo hayo kwa Wakaguzi, Khadija amesema Shirika hilo linalofanya kazi nchi mbalimbali dunia ikiwemo Tanzania pia limejenga uwezo kwa wakaguzi wa OSHA kuhusu masuala ya usalama na Afya, hivyo kupelekea na mabadiliko ya Teknolojia, amesema Shirika hiloa limetoa msaada wa vifaa mbalimbali ambavyo vitatumika kwaajili ya kufanya kaguzi mbalimbali meeno ya kazi.

Nao Washiriki wa Mafunzo hayo kutoka OSHA, wamesema elimu waliyoipata wataitumia kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi, hususan kaguzi mbalimbali watakazokuwa wanazifanya.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2MRBZuD
via

Post a Comment

0 Comments