Ticker

10/recent/ticker-posts

TANZIA:MKUFUNZI WA SHOTOKAN-RYU KARATE AFARIKI DUNIA

Mkufunzi na Mkuu wa Idara ya Ufundi ya JKA/WF-­‐Tanzania kitaifa, pia Mwenyekiti wa Tanzania Shotokan-­‐Ryu Karate-­‐Do Association (TASHOKA) Abdallah Kambi Sensei  amefariki dunia.

Kambi Sensei aliyeingia madarakani tarehe 27 Julai 2019, amefikwa na umautio leo alfajiri katika hospital kuu ya Taifa Muhimbili, alipokua amelazwa kufuatia kusumbuliwa na kifua na tumbo, tangu mwezi August.

Mwenyekiti, JKA/WF-­‐Tanzania Jerome G. Mhagama, amethibitisha kutokea kwa msiba huo, na ameeleza taratibu za maziko ya Kambi Sensei aambaye alijiunga na JKA/WF-­‐Tanzania mwaka 2009 na kuwa mwanafamilia hai wa JKA mpaka umauti unamkuta.
 
Katika hatua nyingine Mhagama ameeleza taarifa nyingine za msiba wa mdau huyo wa mchezo wa Karate, huku wakitarajia majibu wa kikao cha familia ya marehemu.

Ndani ya JKA Kambi Sensei alikuwa mmoja wa Wakufunzi tegemezi mwenye Black Belt 4th Dan-­‐JKA, pia alikuwa na JKA International Licence yenye viwango vya Instructor class C, Judge class D & Examiner class D.
Bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.
Alale mahali pema peponi.



from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2M7wess
via

Post a Comment

0 Comments