Ticker

10/recent/ticker-posts

TAMASHA LA WASAFI KURINDIMA DAR, MASHABIKI WATEGEMEE KUBURUDIKA

 Na. Khadija seif, Michuzi TV
MSANII wa Bongofleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond platnum amewaasa wasanii kutumia Sanaa yao kuongeza pato la taifa.

Akizungumza na waandishi wahabari jijini Dar es salaam wakati akitangaza rasmi ujio wa Tamasha la wasafi kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam amesema kwa mwaka huu imekua neema kwa wasanii wasanaa mbalimbali kupewa nafasi na Waziri wa utalii Hamisi kigangwala kutembelea vivutio vilivopo nchini hasa mlima Kilimanjaro nakujifunza vingi zaidi.

" Tumeanza kupanda mlima Kilimanjaro lakini vingine vingi vitafata lengo likiwa ni kuutangaza utalii wetu kwa nchi za nje ili kujua vitu tulivobarikiwa sisi Kama watanzania,"

Hata hivyo platnum ameeleza ujio huo wa Tamasha utakua ni mara ya Kwanza kwake kutumbuiza Dar  es Salaam kwani hakuweza kufanya hivyo kutokana na kukosa kibali kwa mwaka Jana kutokana na utovu wa nidhamu uliofanyika .

"Niliweza kutumbuiza uwanja wa Taifa katika Tamasha la jamaa lililoandaliwa na Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ,Basi pale niligusa gusa tu balaa lenyewe mashabiki na wapenzi wa lebo ya wasafi (WCB) wajitokeze novemba 9 mwaka huu katika viwanja vya posta jijini Dar es salaam,"

Pia amegusia swala la vijana kupima afya zao nidhahiri wamekua wakipata ushirikiano wakutosha kutoka Taasisi ya kupambana na maambukizi ya virusi vya ukimwi (TACAIDS) na kupewa fursa Kila mkoa kuungana nao na kutoa elimu juu ya kujikinga na kuepuka maambukizi ya ukimwi.

Hata hivyo amefafanua kuwa Wana lengo la kuwa tofauti katika Tamasha la mwaka huu hasa la Dar es salaam na mashabiki wategemee uwepo wa  wasanii wengine wengi kutoka nje ya nchi lengo ni kupata burudani kabambe.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2ouhBGC
via

Post a Comment

0 Comments