Ticker

10/recent/ticker-posts

TAIFA STARS YAWALAZIMISHA SARE RWANDA NYUMBANI KWAO

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' wameilazimisha suluhu  ya 0-0 timu ya Taifa ya Rwanda katika mchezo wa kirafiki uliochezwa leo Nchini Rwanda.

Mchezo huo wa Kirafiki wa Kalenda ya FIFA ulizikutanisha timu hizo Ambapo kila mmoja kushindwa kuona lango la mwenzake.Mchezo wa leo ulikuwa na ushindani mkubwa, timu zote mbili zikisaka ushindi ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya viwango vya FIFA.

Rwanda waliokuwa nyumbani, walionesha uhai mkubwa katika kulisakama lango la Tanzania ila umahiri wa golikipa Metacha Mnata uliweza kuhakikisha lango lake linakuwa salama.

Uwepo wa wachezaji wa Ligi Kuu Tanzania Bara katika safu ya ushambuliaji ya Rwanda ulikua ni mwiba mkali, ila mpaka dakika tisini zimekamilika kwa timu zote kutoka sare ya 0-0.

Wachezaji hao Meddie Kagere, Patrick Sibomana na Haruna Niyonzima ambaye kwa sasa anacheza As Kigali ambapo kabla ya kwenda huko alicheza timu ya Yanga na Simba.Kocha msaidizi wa Stars, Seleman Matola amesema kuwa wachezaji walipambana kupata matokeo ila bahati haikuwa yao.

Matola amesema wachezaji wake walicheza vizuri katika dakika zote 90 wameonesha kiwango kizuri, ila mpira una matokeo matatu kupata sare sio jambo baya ila kwa sasa wanajipanga kwa ajili ya mchezo wa Sudan wa kufuzu kwenda CHAN.

Stars watashuka tena dimbani kucheza dhidi ya Sudan mchezo unaotarajiwa kuwa wa kufa na kupona ambapo Tanzania wanatakiwa wapate ushindi wa goli 2-0 ugenini baada ya mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kupoteza kwa goli 1-0.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2Bd7poU
via

Post a Comment

0 Comments