Ticker

10/recent/ticker-posts

TAARIFA KWA UMMA; KITUO CHA SANAA NA UTAMADUNI KWA VIZIWI TANZANIA( KISUVITA )

KISUVITA NI NINI?

Kituo cha Sanaa na Utamaduni kwaViziwi Tanzania, (KISUVITA), ni asasi isiyo ya kiserikali na isiyolenga faidai na yoongozwa na viziwi kwa ajili ya viziwi, ambao imejikita katika kuimarisha maisha ya wanachama viziwi kupitia sanaa, utamaduni, mawasiliano ya lugha ya alama na uwezeshaji wa kiuchumi.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka2007, KISUVITA imeendeleza vipaji vya viziwi katika Sanaa na utamadun inakusaidia kutengeneza ajira na fursaza mafunzo mbalimbali kwa viziwi nchini Tanzania

TASNIA YA UREMBO NA MITINDO

Kwa kutambulika wajibu wake huo, ndani na nje ya nchi, KISUVITA imekuwa ikipokea mialiko ya kushiriki mashindano mbalimbali ya kimataifa ya urembo na mitindo. Hata hivyo, changamoto ya rasilimali fedha kwa kipindi kirefu tangu ianzishwe ili sababisha ilishindwe kuyashiriki hadi ilipoweza kufanya hivyo mara ya kwanza mwaka huu.

Shukrani za kufanikiwa kushiriki mara ya kwanza tena katika mashindano makubwa ya viziwi ya urembo na mitindo katika ngazi ya kimataifa; Miss & Mister Deaf International yaliyofanyika mjini St. Petersburg, Urusi Julai 5- 17, 2019 zinawaendea wadau kadhaa hasa Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Wizara ya Mali asili na Utalii, Wizara ya Habari na Michezo bila kusahau Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Ushirikiano huo si tu ulituwezesha kushiriki nakufanya vyema baada ya mmoja wa warembo wetu Winfrida Brayson kuingia bora katika mashindano hayo na kushinda kipengele cha utamaduni katika shindano la onesho la mavazi bali pia kung’ara katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni Afrika Mashariki (JAMAFEST) lililomalizika mwishoni mwa Septemba 2019.

Kwa kushiriki kwao, warembo wetu walipata fursa si tu ya kusafiri na kukutana na viongozi kadhaa wa dunia na kuitangaza nchi yetu, bali pia kuwa kiwakilishi na mfano mzuri katika kuhamasisha maadili ya kielimu, kijamii na kiuchumi kwa wanawake na wanaume kupitia tasnia hii popote pale walipo pamoja na kujenga mwamko kwa jamii kuhusu Kiziwi, vipaji na uwezo wao kuleta maendeleo kwa jamii na Taifa lao.

Ushiriki huu ulikuwa wenye wenye tija kwa washiriki wetu binafsi, jamii ya viziwi na Tanzania kwa ujumla, ambao matunda ataonekana siku za usoni. Warembo na waandaaji mbalimbali kutoka ndani na nje ya Afrika na kimatraifa wamepanga kuzuru nchini na hivyo kutoa fursa ya kuchangia kulitangaza Taifa ikiwa mosekta ya utalii. Si hivyo tubali itakuza biashara zetu kwa kuzitangaza kampuni mbalimbali zitakazojitokeza kudhamini matukio ya nayohusu viziwi katika tasnia hii adhimu.


KIFUATACHO BAADA YA KUCHOMOZA KATIKA TASNIA HII

• KISUVITA imeanzisha Shindano la Miss & Mister viziwi Tanzania, ambao watapata tiketi ya kushiriki Miss & Mister viziwi Afrika mjini Nairobi, Kenya mwaka ujao, kabla ya kushiriki Miss & Mister viziwi Dunia ni nchini Marekani

• Inapanga kuwa mwenyeji wa mashindano ya Miss na Mister viziwi ngazi ya Afrika na Dunia siku za usoni

USHIRIKIANO WAKO NI MUHIMU

Hata hivyo, mipango na mikakati hiyo, ambayo si t u itaisaidia jamii ya viziwi bali pia Taifa kwa ujumla wake, itawezekana tukiwa ushirikiano wa wadau mbalimbali kuanzia serikalini hadi sekta binafsi hasa kupitia udhamini.

Kwa sababuhiyo, tunaomba wadau hasa kampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini mashindano au ushiriki wetu katika mashindano ya kimataifa;

• Miss & Mister Deaf Tanzania itakayofanyika mjini Dar es Salaam (Februari 2020)-Dar es salaam

• Miss & Mister Deaf Afrika mjini Nairobi, Kenya (Juni,2020)

• Miss & Mister Deaf International nchini Marekani (Julai,2020)

Katika shindano tutakalo andaa Februari 2020 mjini Dar es Salaam likishirikisha vijana wa kike na kiume ili kupata wa wakilishi wetu, pia litashuhudiwa na warembo na waandaaji wa kimataifa kutoka ndani na nje ya Afrika wakiwamo waandaaji wakuu wa Miss & Mister Deaf International wa Marekani.


FAIDA ZA UDHAMINI

Kuna faida nyingi za kudhamini mashindano haya, kwa kutaja chache ni pamoja na;

• Kulitangaza jina na nembo ya kampuni kupitia vyombo vya habari ndani na nje ya nchi

• Kuhesabiwa ukarimu unaochochea mahusiano mema na jamii hasa watu wenye ulemavu

• Usamaria wema wa kusaidia jamii ya watu wenye ulemavu nchini

• Kuwa sehemu ya mafanikio wachangiaji wa mafanikio ya watu wenye ulemavu hasa katika awamu hii, ambayo Serikali inawapa kipaumbele.

Faida hizo moja kwa moja si tu zitakuza jina la kampuni bali pia kuongeza mapato ya kampuni katika dunia hii ya ushindani wa kibiashara.

Asante sana kwa ushirikiano, wote mnakaribishwa.


Habibu Mrope
Mkurugenzi Mkuu
Kisuvita
+255688744482 -SMS
kisuvita@yahoo.com












from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2BnkrQE
via

Post a Comment

0 Comments