Ticker

10/recent/ticker-posts

SPIKA ATEMBELEA MABANDA MAONESHO YA MAADHIMISHO YA SIKU YA CHAKULA DUNIANI KITAIFA SINGIDA


Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson akipata maelezo ya Ntambo Mahinya mtaalamu wa kupika chakula cha asili kutoka Mbeya alipotembelea banda la vyakula hivyo kwenye maonesho ya maadhimisho ya siku ya chakula duniani yanayofanyika kitaifa mkoani Singida.


Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson akipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa kilimo alipotembelea banda la Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kwenye maonesho ya maadhimisho ya siku ya chakula duniani yanayofanyika kitaifa mkoani Singida.

Dkt. Tulia akipata maelezo jinsi mashine ya kuchakata viazi lishe inavyofanya kazi katika banda la TARI. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Singida, Pasacas Muragiri.
Afisa Kilimo Robert Dimoso Idara ya Usalama wa Chakula Wizara ya Kilimo akimuelezea Dkt.Tulia shughuli zinazofanywa na Idara hiyo.
Mratibu wa Mradi wa Tanipac Wizara ya Kilimo, Clepin Josephat akimurleza Dkt.Tulia Ackson shughuli wanazozifanya.
Dkt. Tulia akipata maelezo ya kilimo cha mapapai.


Afisa Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mary Yongolo akimpatia zawadi ya maziwa Dkt.Tulia Ackson baada ya kutembelea banda la wizara hiyo.
Afisa Lishe Mkoa wa Singida, Teda Sinde akimuelekeza Dkt.Tulia Ackson jinsi ya kupika vyakula vya asili ambavyi ni muhimu katika kuboresha lishe. Kushoto ni Afisa Vijana Mkoa wa Singida, Federick Ndahani.
Dkt.Tulia akipakua chakula cha asili alipotembelea banda la vyakula hivyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt.Rehema Nchimbi akila chakula cha asili kilichotengenezwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI)


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2VJHj6j
via

Post a Comment

0 Comments