Ticker

10/recent/ticker-posts

NBC yatoa wito kwa wazazi kuwafungulia watoto wao Chanua Akaunti ya NBC


BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC), imetoa wito kwa wazazi kote nchini kufungua akaunti maalumu ya watoto ya Chanua pamoja na bima ya elimu ya Educare za benki hiyo ili kuwapa uhakika wa elimu watoto wao pindi wawapo hai ama wasipokuwepo.

Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam hivi karibuni na Kaimu Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa benki hiyo,  Benjamin Nkaka katika hafla waliyoiandaa kwa ajili ya watoto wa wateja wao ikiwa ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha Mwezi wa huduma kwa wateja wa NBC.

Mkurugenzi huyo alisema akaunti ya watoto ya Chanua ya NBC pamoja na bima ya elimu ya educare vitamuwezesha mzazi kuanza kuwekeza kidogodogo kwa ajili ya mtoto wake hivyo kuondoa hofu ya watoto kupata elimu  bora pindi  mzazi  anapoondoka duniani.

“Akaunti ya Chanua na bima ya Educare za NBC ni suluhisho la uhakika kwa elimu ya watoto, wakati mzazi awapo duniani,asipokuwepo au atakapotapa ulemavu wa kudumu, nawashauri wazazi kuwafungulia watoto wenu akaunti hii na kuanza kuwekeza pamoja na bima ya educare zote kutoka NBC,” alisema.

Kuhusu hafla hiyo Bwana Nkaka alisema NBC imekuwa na desturi ya kukutana na wateja wao mara kwa mara ikiwa ni moja ya azma yao ya kusogeza huduma zao karibu na wateja wao hivyo licha ya kuwaeleza watoto  walioambata na wazazi wao bidhaa mbalimbali zinazotolewa na benki hususan zinazowalenga watoto, lakini pia watoto walishiriki burudani za aina mbalimbali jambo ambalo ni muhimu katika malezi ya watoto.

“NBC imekuwa ikibadilika siku hadi siku tukitumia njia mbalimbali katika kuwafikia wateja wetu, licha ya kuwa na mtandao mpana wa matawi lakini pia tumeanzisha NBC Kiganjani inayomuwezesha mteja kupata huduma mbalimbali za kibenki kwa kupitia simu yake ya mkononi.


“Lakini hii haitoshi NBC inao mtandao mkubwa wa mawakala wake wakitoa huduma mbalimbali za kibenki nchini kote, lakini hivi karibuni tumeingia ushirika na Shirika la Posta ambapo wateja wetu wanaweza kupata huduma zetu za kibenki katika ofisi zote za shirika hilo mahali kote nchini,” aliongeza mkurugenzi hiuyo.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2OPFOlE
via

Post a Comment

0 Comments