Ticker

10/recent/ticker-posts

NAIBU SPIKA DKT. TULIA ACKSON AWATAHADHARISHA WATANZANIA KUHUSU MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI


Baada ya Mahakama ya Rufani Tanzania kubatilisha vifungu vya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 inayoruhusu mtoto wa kike kuolewa chini ya miaka 18. jana  October 24, 2019 Naibu Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson akifungua Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Uzazi na Malezi Bora Tanzania (UMATI) uliofanyika Jijini Dodoma amesihi Watanzania kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu athari za ndoa na mimba za utotoni.

“Watu wote tungependa ile Hukumu ya ilivyotoka tu, yaani watu miaka 18 ndio waanze kufikiri ndoa. Sote tunafahamu hata miaka 18 sio kwamba ndio yupo tayari kwa ajili ya ndoa lakini niwaombe sisi tuendelee kuweka mkazo kwenye mafunzo kwa vijana wetu wenye umri mdogo kwamba hata ile miaka 18 yeye haimtoshi kuanza kubeba familia ili pamoja na haya mengine tusianze sasa tumemaliza la ndoa za utotoni tunajikuta tunaendeleza mimba za utotoni”

“Kwa maana hivi ni vitu viwili tofauti japokuwa kuna mahali huwa vinakutana. Ndoa za utotoni zinapelekea mimba za utotoni lakini sio mimba zote za utotoni zinasababishwa na ndoa za utotoni”-Dkt. Tulia Ackson


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2WgtRqS
via

Post a Comment

0 Comments