Ndege Inatua Leo Katika Ardhi ya Tanzania ni Ndege ya 8 KWENYE Orodha ya Ndege za AIR TANZANIA
1. Boeing 787-8 Zipo 2
2. Forker 50 Ipo 1
3. Bombardier Dash 8-400 Zipo 3
4. Bombardier Dash 8-300 Ipo 1
5. Airbus A220-300 Zipo 2
Ndege Hii Mpya Imesajiliwa Kwa Usajili Namba 5H-TCJ na Imepewa Brand Name ya Visiwa vya RUBONDO ISLAND Vilivyopo Mkoani Mwanza Vyenye Ukubwa wa Kilometre za Mraba 456.8 Sawa na Kushabihiana Ukubwa wa Manispaa ya KINONDONI Mkoa wa DAR ES SALAAM
Ndege Mpya ya Air TANZANIA Boeing 787-8 Ina Uwezo wa Kutembea Kilometres 13620 Sawa na saa zaidi ya 12 Hewani Bila ya Kusimama
Inabeba Lita 101,000 za Mafuta na Ina Ukubwa wa MITAA 56.72 Yaani Ni Sawa na Nusu ya Uwanja wa Mpira wa Miguu
Inabeba Jumla ya Abiria 262
Ina Uwezo wa Kubeba Uzito wa Tani 227 Yaani 227,930Kg Wakati wa Kupaa Uzito wa Hujumuisha Uzito wa Chombo,Mizigo,Mafuta na Inapotua Inatakiwa Iwe na Tani 172 za Uzito, Hii Inatokana na Kupungua Kwa Kiasi Cha Mafuta Wakati wa Kutua .
Sifa ya Ndege Hii Ina Uwezo Mkubwa wa Kuhimili Hali Nzito ya Hewa Ikiwa KWENYE Umbali Mrefu Kwenda Juu
Leo Tunaipokea Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JNIA
Mgeni RASMI ni Mhe RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, H:E Dr JOHN POMBE MAGUFULI
from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2oiT9rB
via
0 Comments