Ticker

10/recent/ticker-posts

JAFO AZIAGIZA HALMASHAURI ZOTE NCHINI KUFUNGUA AKAUNTI MAALUM YA FEDHA ZA WANAWAKE, VIJANA NA WALEMAVU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Serikali Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jafo akiongea wakati wa kufunga Kongamano la Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wataalam wa sekta ya maendeleo ya jamii lilofanyika jijini Dodoma.Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW

*******************************

Na Mwandishi Wetu Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bw. Suleiman Jafo ametao mwezi mmoja kwa Halmashauri zote Nchini kuhakikisha zinafungua akaunti maalum ya Benki kwa ajili ya fedha za maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Waziri Jafo ametoa agizo hilo jana wakati akifunga kongamano la wataalam wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii jijini Dodoma nakuwataka wataalam hao kuhakikisha wanakwenda kusimamia zoezi hilo na kukamilisha katika kwa kipindi cha mwezi mmoja.

‘’Natoa maagizo ifikapo Novemba, 30 kila Halmashauri Nchini iwe imefungua akaunti maalum ya Benki kwa ajili fedha ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa kuwa fedha zikitolewa katika mfumo wa sasa zinakuwa kama zinaelea’’. Alisitsiiza Waziri Jaffo.

Aidha Waziri Jafo aliongeza kuwa fedha hizi zinapotelewa bila akaunti hiyo inakuwa vigumu kwa serikali kuzifanyia tathimini hivyo kuwaimiza wataalam wa sekta ya maendeleo ya jamii katika Halmashauri zao kuhakikisha wanatekeleza agizo hilo ili malengo na matumizi ya fedha hizo yaweze kufanyiwa tathimini.

Pamoja na kutoa agizo hilo Waziri Jafo pia ameongeza kuwa ili jamii iweze kuleta mabadiliko yanayotakiwa suala la kutumia wataalam wa maendeleo ya jamii halikwepiki kwa sasa wakati jamii inataka mabadiliko ya haraka kuelekea Tanzania ya viwanda.

Wataalam hawa ni chachu ya mabadiliko na katika mashirika makubwa duniani wataalam wa maendeleo ya jamii wamekuwa wakitumiwa sana ili kuleta mabadiliko katika nyanja mbalimbali na wamekuwa msaada mkubwa kitaifa na kimataifa.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu katika hotuba yake kwa Waziri huyo aliongeza kuwa kongomano hilo lilikuwa na mjadala mkubwa kuhusu kuhamasisha jamii kujiletea maendeleo kwa kutumia istilahi zilizoko katika jamii akitolea mfano wa istilahi maalufu kwa mikoa ya ya kati ijulikanayo kama Msalagambo.

Aidha Dkt. Jingu aliongeza kuwa matokeo ya kongamano hilo pia nikuwafanya wataalam hao wajione kuwa wao ni chachu ya maendeleo katika kuhamasisha wananchi kuwa na ari ya kujiletea maendeleo.



Wakati huo huo Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka TAMISEMI aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara yake katika Kongomano hilo Bw.John Miayo Cheo aliwataka wataam wa maendeleo ya jamii kutumia taaluma yao kuhamasisha wananchi kugombea nafasi za uongozi ili waweze kuwa viongozi wa kufuatia uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa. 

Wataalamu wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii wamekutana Jijini Dodoma katika Mkutano Mkuu wao wa mwaka kwa lengo la kukumbushana majukumu yao lakini pia kupata maarifa mapya kutoka mada mbalimbali zitakazotolewa katika mkutano huo wa siku nne


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/33Z5Ve0
via

Post a Comment

0 Comments