Ticker

10/recent/ticker-posts

HALI YA FOLENI KWA SASA JIJINI DAR, MVUA INAENDELEA KUNYESHA

JIJI la Dar es Salaam leo hali ya mvua imekuwa kizungumkuti na usafiri nao umekuwa shida kutokana na maji kutatapakaa kila mahali na hivyo kusababisha usafiri kuwa Mgumu kwa kuwa na foleni.

Kwa wanaopita barabara mbalimbali za jiji la Dar es Salaam kuelekea eneo lenye ofisi nyingi la Posta chukueni tahadhali kabla ya kutoka kwa kuangalia ni barabara itakayokuwa na unafuu wa kufika eneo hilo.

Picha hapo juu inaonyesha rangi mbalimbali katika barabara za hapa mjini.
Rangi hizo  zinaashiria namna barabara ilivyo kwa sasa kwakuwa rangi nyekundu zaidi ya nyingine zote inaonyesha foleni ambayo inaenda lakini taratibu.

Hivyo chukua maamuzi ya kubadilisha njia kwa kuangalia yenye unafuu wa kufika mahali ambapo unataka kufika bila kupoteza muda mwingi.


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2VMTyio
via

Post a Comment

0 Comments