Ticker

10/recent/ticker-posts

BALOZI ALI KARUME AFUNGUA KONGAMANO LA VIJANA KITAIFA MKOANI LINDI



Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Balozi Ali Abeid Karume akizungumza na Vijana walioshiriki Kongamano la 17 la vijana kitaifa lililofanyika Mkoani Lindi katika Ukumbi wa Kagwe Oktoba 11, 2019 ikiwa ni kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Baadhi ya vijana wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Balozi Ali Abeid Karume (hayupo pichani) wakati wa kongamano la vijana walililowakutanisha vijana kujadili mchango wa Baba wa Taifa katika maendeleo ya Bara la Afrika.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akieleza jambo wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo lililofanyika Mkoani Lindi katika Ukumbi wa Kagwe Oktoba 11, 2019.


Bi. Aisha Kombo kutoka Zanzibari akiimba utenzi kuhusu waasisi wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Hayati Mzee Abeid Karume.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akisikiliza utenzi uliokuwa ukiibwa na Bi. Aisha Kombo. Kulia ni Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Balozi Ali Abeid Karume. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi.


Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Godfrey Zambi akieleza jambo wakati wa Kongamano hilo la Vijana Kitaifa. Kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama


Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Kenya Bi. Rose Mugu akitoa taarifa fupi kuhusu ushuhuda wa vijana kutoka nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika juu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. 


Kikundi cha International Youth Fellowship wakitoa burudani wakati wa kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Kagwe, Mkoani Lindi.


Bw. Usman Mchinja mwakilishi kutoka Shirikisho la Vyuo Vikuu Tanzania (TAHLISO) akielezea mchango wa vijana katika taifa wakati wa Kongamano la vijana lilifanyika Mkoani Lindi.



PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU

(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)


from MICHUZI BLOG https://ift.tt/2MakKEI
via

Post a Comment

0 Comments